Ticker

6/recent/ticker-posts

UGONJWA WA CHANGO LA UZAZI(chanzo,dalili na Tiba)



  CHANGO LA UZAZI

• • • • •

UGONJWA WA CHANGO LA UZAZI(chanzo,dalili na Tiba)


Ugonjwa wa chango la uzazi, umekuwa ugonjwa ambao hutesa sana wanawake wengi kwa hivi sasa, japo hata wanaume pia huweza kupatwa na ugonjwa wa chango kama wengine ambavyo hawafahamu kabsa hili.


Madhara ya ugonjwa wa chango kwa mwanamke ni makubwa na huhusisha madhara mbali mbali kama vile; Mwanamke kupoteza uwezo wa kubeba mimba, mimba kuharibika zenyewe,maumivu makali ya tumbo N.K


CHANZO ZA UGONJWA WA CHANGO LA UZAZI


- Chango la uzazi kwa mwanamke hutokea pale ambapo vifuko vya mayai yaani Ovaries kuwa na shida, Shida hii huhusisha vifuko vya mayai(ovaries) kupoteza uwezo wake wa kawaida wa kuzalisha mayai na kufanya yakue ndani ya wakati wake,kitu ambacho hupelekea baadhi ya wanawake kukosa hedhi,hedhi kutokuwa na mpangilio maalumu au kupoteza uwezo wa kubeba mimba.


- Mabadiliko ya vichocheo vya mwili kama vile; Uzalishaji wa kiwango kikubwa wa kichocheo aina ya Prolactin kwenye damu hali ambayo hudhibiti na kuzuia uzalishwaji wa kichocheo cha Estrogen, Mvurugiko wa vichocheo vya Lutenizing hormones na Folicle stimulating hormones kwenye ubongo N.K


DALILI ZA UGONJWA WA CHANGO LA UZAZI


- Mwanamke kupata maumivu makali ya tumbo


- Mwanamke kupata maumivu makali ya kiuno


- Mwanamke kupata maumivu makali ya mgongo


- Joto la mwili kupanda au kuwa na homa pale mwanamke anapokaribia hedhi


- Mwanamke kupatwa na maumivu makali ya tumbo wakati wa hedhi au anapokaribia hedhi yake


- Mwanamke kuwa na uchovu mkubwa wa mwili kipindi cha hedhi


- Kukosa mpangilio maalumu wa hedhi


- Kushindwa kubeba mimba


- Mimba kuharibika zenyewe

N.K


MATIBABU YA UGONJWA WA CHANGO LA UZAZI


- Zipo dawa mbali mbali za kudhibiti dalili za ugonjwa huu lakini sio za kuondoa kabsa shida hii kwa hospitalin. 


Hivo basi kama mwanamke atapata maumivu makali wakati wa hedhi atapewa dawa za maumivu, kama mwanamke anashindwa kuzalisha mayai atapewa dawa za kuzalisha mayai N.K



KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments