Ticker

6/recent/ticker-posts

KUWA NA TATIZO LA DUTU ZA SEHEMU ZA SIRI



 SEHEMU ZA SIRI

• • • • •

KUWA NA TATIZO LA DUTU ZA SEHEMU ZA SIRI


Tatizo hili ni miongoni mwa matatizo ambayo yapo katika kundi la magonjwa ya zinaa au magonjwa yanayoenezwa na kusambazwa kwa njia ya kufanya mapenzi yasio salama au Ngono Zembe.


CHANZO CHA TATIZO HILI LA DUTU ZA SEHEMU ZA SIRI


- Tatizo hili husababishwa na maambukizi ya virusi jamii ya Human papilloma au virusi wajulikanao kama HUMAN PAPILLOMA VIRUS(HPV) wakati wa Kufanya mapenzi


DALILI ZA TATIZO HILI NI PAMOJA NA;


- Ngozi ya sehemu za siri kuanza kuwa na vitu kama vipele lakini vigumu


- Kuwa na dutu maeneo mbali mbali ya mwili wa binadamu kama vile sehemu ya haja kubwa,kwenye uke au uume.



MATIBABU YA TATIZO HILI LA KUWA NA DUTU ZA SEHEMU ZA SIRI


- Tiba sahihi na salama kwa tatizo hili huhusisha aina ya upasuaji mdogo au operation ya kuziondoka hizi dutu sehemu husika,pamoja na mgonjwa kupewa dawa za kudhibiti hali ya maumivu pamoja na kuzuia sehemu ambayo kafanyiwa upasuaji isishambuliwe na wadudu au magonjwa mengine.



KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.








Post a Comment

0 Comments