Ticker

6/recent/ticker-posts

UGONJWA WA MAFUA YA AVIAN(chanzo,dalili na tiba)



 MAFUA

• • • • •

UGONJWA WA MAFUA YA AVIAN(chanzo,dalili na tiba)


Ugonjwa wa mafua ya avian ni ugonjwa wa mafua ambao husababishwa na virusi ambao hupatikana kwa ndege(Avian) na kwa kitaalam hujulikana kama Avian flu au Avian influenza.


Ugonjwa huu kwa asilimia kubwa hushambulia jamii ya ndege,kuku n.k japo kuna case chache pia ziliripotiwa kwamba ugonjwa huu huweza kushambulia hata binadamu pia.


DALILI ZA UGONJWA WA MAFUA YA AVIAN KWA BINADAMU


- Mgonjwa kupatwa na mafua makali


- Mgonjwa kupatwa na maumivu makali ya tumbo


- Mgonjwa kuvimba macho pamoja na macho kuwasha


- Joto la mwili la mgonjwa kuwa juu au mgonjwa kuwa na homa


- Mgonjwa kupata kikohozi


- Mgonjwa kupata maumivu ya misuli,viungo pamoja na joints


- Mgonjwa kuhisi kichefuchefu pamoja na kutapika


- Mgonjwa kukosa hamu ya kula pamoja na ladha ya chakula kupotea


- Mgonjwa kuanza kuharisha


- Mgonjwa kupata shida ya upumuaji


- Mgonjwa kukosa pumnzi ya kutosha


- Mwili wa mgonjwa kutetemeka au kutingishwa hali ambayo kwa kitaalam hujulikana kama fits au seizures.


- Mgonjwa kupata maumivu makali ya kichwa


- Mgonjwa kupatwa na hali ya kizunguzungu

N.k


MATIBABU YA UGONJWA WA MAFUA YA AVIAN


Kama ilivyo kwa matibabu ya magonjwa mengine mengi ambayo husababishwa na virusi, tiba huwa katika kudhibiti dalili za ugonjwa kama vile; mgonjwa kupewa dawa za kutuliza mafua,maumivu n.k


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments