Ticker

6/recent/ticker-posts

Dalili za ugonjwa wa kipanda uso(migraine)



 KIPANDA USO

• • • • • •

Dalili za ugonjwa wa kipanda uso(migraine)


Kipanda uso ni tatizo ambalo huhusisha mtu kupatwa na maumivu makali sana ya kichwa ambayo hutokana na sababu mbali mbali kama vile;


hali ya kutanuka kwa mishipa ya damu kichwani kama vile mishipa aina ya Artery, 


mabadiliko ya mfumo wa damu yaani Blood stream na mabadiliko ya vichocheo kama vile; kichocheo aina ya Serotonin ambacho huhusika na kudhibiti kiwango cha maumivu kwenye mfumo wa fahamu.


Vyote hivi huchangiwa na sababu mbali mbali kama vile;


✓ Mtu kuwa na msongo wa mawazo


✓ Matumizi ya pombe kali kupita kiasi


✓ Kunywa vinywaji vyenye caffeine nyingi kama kahawa N.k


✓ Kukosa muda wa kutosha wa kulala


✓ Matumizi ya dawa mbali mbali kama vile; vidonge vya uzazi wa mpango n.k


✓ mabadiliko ya hali ya hewa mfano; Kuwa na jua kali pamoja na joto sana

N.k


DALILI ZA TATIZO LA KIPANDA USO(MIGRAINE) NI PAMOJA NA;


Siku moja au mbili kabla ya tatizo hili kutokea,mtu huweza kupata mabadiliko kama vile;


• Kuanza kupata choo kigumu


• Kupoteza mood


• Shingo kukakamaa


• Kiu ya maji kuongezeka sana pamoja na mtu kukojoa sana


• Mtu kupiga miayo sana


• Kuanza kupata shida ya kutokuona vizuri au kuona marue rue


NDIPO BAADAE dalili zingine hujitokeza mfano;


- Maumivu makali ya kichwa


- Mshipa kucheza cheza  upande mmoja wa kichwani


- Kupatwa na hali ya kichefuchefu pamoja na kutapika


- Mtu kupata kizunguzungu kikali


- Kuhisi sauti za makelele masikioni


- Kupata shida ya kuongea


- Mwili kutetemeka


- Mwili kukosa nguvu


- Dalili za kuchanganyikiwa

N.K


MATIBABU YA TATIZO HILI LA KIPANDA USO


• Zipo dawa mbali mbali za kuondoa maumivu haya kama vile; Ibuprofen, Paracetum N.k


japo endapo mtu hupata dalili mbaya zaidi kama kushindwa kuongea,mwili kutetemeka, n.k ni vizuri kuwaona wataalam wa afya.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments