Ticker

6/recent/ticker-posts

Ugonjwa wa SAFURA,chanzo,dalili na Tiba yake



   SAFURA

• • • • •

Ugonjwa wa SAFURA,chanzo,dalili na Tiba yake


Ugonjwa wa Safura ni ugonjwa ambao huwapata watu wengi hasa watoto wadogo.


CHANZO CHA UGONJWA WA SAFURA


- Ugonjwa wa Safura ni ugonjwa ambao husababishwa na Mashambulizi ya Minyoo aina ya HOOKWORMS


DALILI ZA UGONJWA WA SAFURA Ni pamoja na;


✓ Mtu kukosa hamu ya chakula


✓ Baadhi ya watu kula kupita kawaida


✓ Mwili kudhoofika ikiwa ni pamoja na kukonda sana


✓ Mwili kukosa nguvu kabsa


✓ Misuli ya mwili kuwa dhaifu


✓ Kupata maumivu ya tumbo mara kwa mara


✓ Mgonjwa kuharisha mara kwa mara


✓ Kuhisi dalili ya Minyoo njia ya haja kubwa wakati wa kujisaidia


✓ Nywele kunyonyoka zenyewe


✓ Kupata dalili zote za kuishiwa na damu yaani Anemia

N.k



MATIBABU YA UGONJWA WA SAFURA


Ugonjwa huu wa safura hutibiwa kwa dawa mbali mbali,ikiwa ni pamoja na dawa za Minyoo jamii ya Albendazole,mebendazole(kwa wajawazito) N.k


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.





Post a Comment

0 Comments