Ticker

6/recent/ticker-posts

ATHARI ZA UPWEKE(soma kujua hii)



UPWEKE

• • • • •

ATHARI ZA UPWEKE(soma kujua hii)


 Pamoja na athari zingine,upweke hudhoofisha sana kinga ya mwili,huharibu mzunguko wa kawaida wa usingizi,husababisha mtu apate sonona huchangia kwa kiasi kikubwa kutokea kwa magonjwa ya moyo.

-

Utafiti wa John Cacioppo unaeleza kuwa upweke unaweza kusababishwa na asili ya binadamu mwenyewe tangu kuzaliwa kwake au hata kutokana na matukio mbalimbali yanayotokea kwenye maisha ya kila siku ya binadamu.


Upweke unaotokana na vifo vya wapendwa wetu,kuachika katika uhusiano wa mapenzi,kufilisika pamoja na kukosa kazi (au kufukuzwa kazi) ndiyo huleta madhara makubwa sana kwa mhusika hasa vifo vya ghafla au hata kuupunguza umri wa kuishi wa mhusika.

-

Watu wenye upweke hawapaswi kubezwa,wanahitaji kusaidiwa kwa hali na mali maana hali hii inaweza hata kuondoa uhai wao.


Tusaidiane hasa katika nyakati ngumu kama hizi,zungumza nao,pia onesha kuwasaidia kwa kadri utakavyoguswa!


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments