Ticker

6/recent/ticker-posts

JINSI YA KUPUNGUZA TUMBO(afyatips)



 TUMBO

• • • • •

JINSI YA KUPUNGUZA TUMBO(afyatips)


Kwa hivi sasa watu wengi hupambana na njia mbali mbali za kupunguza matumbo yao hasa wadada ili kuonekana warembo zaidi, na kuvaa nguo ipendeze, Hivo basi huwapelekea kutumia njia mbali mbali ili kupunguza tumbo, huku zingine zikiwa sahihi na zingine zikiwa hatari zaidi kwa afya zao. Hapa kuna baadhi ya mambo ya kuzingatia wakati unahitaji kupunguza tumbo lako,


1. Hakikisha unapendelea zaidi kula vyakula pamoja na matunda yenye nyuzi nyuzi au Fibers kama vile machungwa,maembe,maparachichi n.k


2. Epuka kula vyakula vyenye mafuta zaidi ikiwemo chips


3. Epuka matumizi ya pombe kupita kiasi


4. Kula vyakula vyenye kiwango kikubwa cha PROTEIN na sio kiwango kikubwa cha MAFUTA mfano; Maharage n.k


5. Punguza au epuka kabsa kuwa na msongo wa mawazo,watu wengi hawajui kwamba msongo wa mawazo huweza kusababisha tatizo la kuongezeka kwa tumbo au hata uzito kwa baadhi ya watu


6. Epuka kula vyakula vyenye kiwango kikubwa cha sukari


7. Fanya mazoezi ya mwili kila siku,angalau kwa dakika 30 au Nusu saa kila siku


8. Hakikisha unapata muda wa kutosha wa kupumzika pamoja na kulala


9. Unaweza kupendelea kula vyakula jamii ya samaki zaidi huku ukiepuka mafuta mengi


10. Japo juice za matunda ni nzuri sana, ila baadhi zina kiwango kikubwa sana cha sukari,hivo epuka juice kama hizi


11. Kunywa chai ya kijani maarufu kama GREEN TEA, najua wengi wenu hamjawahi kusikia hii,ila ipo na watu wanaitumia hivo ulizia itakusaidia pia.


12. Pamoja na Tips zingine za Afya


KUMBUKA; kufunga mkanda tumboni ili tumbo lipungue au kushinda na njaa kila siku huweza kuwa hatari kwako na sio njia salama ya kupunguza tumbo


• Soma pia: Jinsi ya Kupunguza Uzito wa Mwili


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments