Ticker

6/recent/ticker-posts

TATIZO LA KUPOTEZA UWEZO WA KUNUSA



 PUA/HARUFU

• • • • • •

TATIZO LA KUPOTEZA UWEZO WA KUNUSA


Tatizo hili la kupoteza uwezo wa kunusa au mtu kusikia harufu ya kitu chochote ambapo kwa kitaalam hujulikana kama ANOSMIA hutokea sana kwa watu wengi hivi sasa, na kwa asilimia kubwa huendana na tatizo la kupoteza uwezo wa kutambua ladha ya kitu chochote kama chakula n.k, je chanzo chake ni nini?


CHANZO CHA TATIZO LA KUPOTEZA  UWEZO WA KUNUSA NI PAMOJA NA;


1. Kuvimba au kuziba kwenye pua kutokana na sababu mbali mbali kama vile; Uwepo wa uvimbe, tatizo la Nasal Polyps, Matatizo kwenye mifupa ya puani yaani Bone deformities n.k


hali ambayo hupelekea pua kushindwa kuhisi harufu pamoja na kuathiri mfumo mzima wa kutuma taarifa zinazohusiana na harufu kutoka puani kwenda kwenye ubongo.


2. Tatizo la kuharibika kwa ubongo pamoja na nerves kutokana na sababu mbali mbali kama vile;


- Kupata ajali na kugongwa kichwani


- tatizo la uvimbe kwenye ubongo au Brain tumors


- Umri kuwa mkubwa zaidi


- Ugonjwa kama vile Alzheimers disease


- Matatizo ya mvurugiko wa vichocheo mwilini


- Matatizo ya tezi la thyroid kama vile underactive thyroid n.k


- Matumizi ya baadhi ya dawa kama vile viuwajisumu yaani antibiotics,dawa za presha n.k


- Ugonjwa wa kisukari


- Tatizo la kifafa au Epilepsy


- Matatizo kama vile multiple sclerosis


- Kuumia kichwani au kwenye ubongo


- Kufanyiwa upasuaji unaohusisha ubongo


- Kupata huduma ya mionzi yaani Radiotherapy


- Matumizi ya pombe kwa muda mrefu


- Tatizo la kiharusi au Stroke n.k


3. Sababu zingine ni kama vile;


- Tatizo la maambukizi ya magonjwa kama vile Sinus infections


- Tatizo la mafua makali au ya mara kwa mara, hii huchangia kwa asilimia kubwa mtu kushindwa kuhisi harufu ya kitu chochote


- Uvutaji wa sigara


- Tatiizo la Mzio au Allergy kama vile; Allergic rhinitis n.k


- Tatizo la kuziba pua kwa muda mrefu n.k


MATIBABU YA TATIZO LA KUPOTEZA  UWEZO WA KUNUSA


- Watu wenye tatizo hili huweza kupata tiba mbali mbali kulingana na chanzo cha tatizo hili, ikiwa ni pamoja na; matumizi ya dawa jamii ya

• DECONGESTANTS kama vile Phenylephrine


• au Jamii ya ANTIHISTAMINES


• Dawa jamii ya Steroids-nasal sprays


• Antibiotics mbali mbali


• Dawa za Allergies kama vile CETRIZINES n.k


KUMBUKA DAWA HIZI HUWEZA KULETA MAUDHI MADOGO MADOGO MWILINI BAADA YA MATUMIZI YAKE KAMA VILE;


✓ Mtu kuhisi kizunguzungu


✓ Hamu ya chakula kuisha kabsa


✓ Mtu kuhisi usingizi mzito au kukosa kabsa usingizi


✓ Presha kupanda juu


✓Hali ya kuwa na wasiwasi,kutokutulia n.k


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments