Ticker

6/recent/ticker-posts

Inawezekana kuutokomeza kabisa UKIMWI ifikapo mwaka 2030



Umoja wa Mataifa umesema inawezekana kuutokomeza kabisa UKIMWI ifikapo mwaka 2030 endapo tu Mashirika ya Kijamii na Watu walioko katika mstari wa mbele kupambana na ugonjwa huo watawezeshwa.

Ripoti ya Shirika hilo imeeleza kuwa ingawa Dunia bado haijakomesha kabisa UKIMWI kama tishio la afya kwa umma kuna matumaini ya lengo hilo kufikiwa toka lilipotangaza mpango huu mwaka 2015.

Kwa sasa kuna Watu milioni 39 wanaoishi na virusi vya HIV Duniani kote na kati ya hao milioni 20.8 wako Mashariki na Kusini mwa Afrika huku wengine milioni 6.5 wakiwa Asia na Pasifiki huku milioni 9.2 yao wakiwa hawana dawa za kupunguza makali ya virusi hivyo, imeripoti @dw_kiswahili



Post a Comment

0 Comments