Ticker

6/recent/ticker-posts

Dawa ya red eyes,Ifahamu dawa ya macho mekundu hapa



Dawa ya red eyes,Ifahamu dawa ya macho mekundu hapa

Je unahitaji kutumia Dawa ya red eyes? na kama ni hivo ni ipi Dawa ya red eyes?

Ingawa ugonjwa wa red eyes huiisha au kuondoka wenyewe, kuna wakati unahitaji matibabu maalumu kutoka kwa wataalam wa afya ikiwa umekusababishia madhara Zaidi.

Hakikisha unaongea na wataalam wa afya Ili kupata Dawa ya red eyes haraka Zaidi ikiwa unapata hali hizi hapa;

– Unahisi maumivu makali sana kwenye Macho

– Uwezo wako wa kuona umeathiriwa na ugonjwa wa Red Eyes

– Macho yako yanaogopa mwanga

– Macho yanazidi kuwa mekundu siku hadi siku badala ya kupungua wekundu

– Unapatwa na Homa

– Macho kutoa Usaha badala ya tongotongo n.k

Dawa ya red eyes

Hizi hapa ni jamii ya Dawa ambazo huweza kutumika kutibu Ugonjwa wa Red Eyes Duniani, si dawa Zote utazipata hapa Tanzania,

Hivo ni muhimu kuwasaliana kwanza na wataalam wa afya au tuwasiliane hapa afyaclass ili kupata Dawa ya red eyes sahihi na inayopatikana hapa kwetu Tanzania.

Kumbuka; Matibabu ya ugonjwa wa red eyes huhusika na chanzo husika.

Dawa ya red eyes ni pamoja na;

✓ Naphazoline, ambayo hupatikana kwenye dawa jamii ya Clear Eyes Itchy Eye Relief.

Naphazoline ni dawa jamii ya decongestant ambayo hutibu macho mekundu(red eyes) ikiwa chanzo chake ni mzio au allergic reactions.

✓ Tetrahydrozoline, ambayo hupatikana mfumo wa matone kama vile Visine. Tetrahydrozoline ni dawa jamii ya decongestant kama vile naphazoline,

Hivo huondoa wekundu kwenye macho ambao hutokana na Mzio(allergy, exhaustion, and irritation).

✓ Eye lubricant drops. Pia zipo dawa za macho ambazo kazi yake kubwa ni kuwa kama vilainishi machoni, hizi pia huweza kutumika kama Dawa ya red eyes.

✓ Dawa ya red eyes, Haya ni matibabu mengine ya Ugonjwa wa red eyes;

Ikiwa umepata shida ya red eyes kwa sababu kama hizi allergies, conjunctivitis, au blepharitis, unaweza kufanya matibabu haya rahisi kwako;

SOMA ZAIDI HAPA: Kuhusu Dawa Za Ugonjwa wa macho

(1) Kutumia vitu vya baridi(Apply a cool compress). kuweka kitu cha baridi juu ya macho ukiwa umefunika macho yako huweza kusaidia kupunguza dalili za wekundu na kuvimba kwa macho.

(2) Tumia baadhi ya dawa(Take over-the-counter (OTC) medications).

Kama nilivyokwisha kueleza,dawa jamii ya antihistamines au decongestants huweza kutumika kama dawa ya Red eyes, ambapo husaidia kupunguza na kuondoa  dalili za wekundu wa macho.

Pia dawa kama vile ibuprofen pamoja na acetaminophen huweza kutumika kupunguza maumivu na Uvimbe.

(3) Epuka vitu vyote vinavyoweza kuingia machoni(Avoid irritants).

Hapa tunazungumzia vitu kama vile Vumbi, Moshi, pollens, chemical fumes n.k.

(4) Hakikisha unanawa mikono(Wash your hands).

Hakikisha unanawa mikono yako mara kwa mara kwa kutumia maji safi tiririka na Sabuni.

Epuka kabsa kugusa macho yako au eneo la karibu na macho yako hasa ukiwa hujanawa mikono yako.

(5) Epuka makeup au kuvaa miwani.

Epuka kutumia makeup au kuvaa miwani kam ikiwezekana mpaka dalili za ugonjwa wa red eyes ziondoke.

(6) Epuka kutazama vitu kama Simu,TV, au computer kwa muda mrefu.

Kutumia muda mwingi mbele ya kompyuta, TV au skrini ya simu kunaweza kusababisha macho kuwa na mkazo zaidi(eyestrain) na kuwa makavu, kwa hivyo jaribu kupunguza muda wako wa kutumia kifaa kama hivi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Ugonjwa wa Macho Mekundu(RED EYES),chanzo,dalili na Matibabu



Post a Comment

0 Comments