Ticker

6/recent/ticker-posts

Fundi anaswa na umeme na kufariki alipokuwa akirekebisha jokofu huko Ogun



Fundi anaswa na umeme na kufariki alipokuwa akirekebisha jokofu huko Ogun.

Fundi aliyetambulika kama Sanjo Adeosun amenaswa na umeme kwenye Mtaa wa Power katika eneo la Abule-Iroko katika Jimbo la Ogun nchini Nigeria,

Alipotaftwa mmiliki wa friji hiyo, Amos Alexander, aliambia Kitengo cha Polisi cha Sango-Ota kuwa fundi huyo alifariki dunia wakati wa ukarabati wa friji.

Msemaji wa Kamanda wa Polisi wa Jimbo, Omolola Odutola, ambaye alithibitisha tukio hilo kwa Punch  Jumapili, Januari 7, 2024, alisema mwili wa Adeosun ulikuwa umehifadhiwa katika Hospitali Kuu ya Ifo kwa ajili ya uchunguzi wa maiti.

“Tukio hilo lilipofikishwa kwa watu wetu, walikimbia hadi eneo la tukio na kumpeleka mtu huyo hospitali ambapo daktari wa zamu alitangaza kufariki dunia.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha maiti cha hospitali. Familia yake imetafutwa kuhusu tukio hilo,” PPRO ilisema.



Post a Comment

0 Comments