Connect with us

Magonjwa

kunywa dawa na maziwa

Avatar photo

Published

on

kunywa dawa na maziwa

Dawa ambazo haziruhusiwi kuchanganya na maziwa

Fahamu kwamba; Maziwa yanaweza kuingiliana na jinsi madini chuma yanavyofyonzwa tumboni, na kalsiamu inayopatikana katika bidhaa za maziwa inaweza kuzuia mwili kunyonya antibiotics/viuavijasumu vya tetracycline na ciprofloxacin pamoja na dawa za matatizo ya tezi, kwa hivyo utapata chini ya kiwango katika mwili wako.

Haya hapa ni maelezo kuhusu dawa ambazo haziruhusiwi kuchanganywa na maziwa;

1. Dawa Za Tezi la Shingoni(Thyroid Medication)

Watu wengi hutumia dawa za kutibu matatizo ya tezi kama vile tatizo la hypothyroidism, Tatizo ambalo huhusisha tezi hili la shingoni kutokufanya kazi vizuri na kuzalisha kiwango cha kutosha cha vichocheo vinavyojulikana kama thyroid hormone.

Zipo baadhi ya dawa za kutibu tatizo hili ambazo haziruhusiwi kutumika pamoja na maziwa, dawa hizo ni pamoja na;

  • levothyroxine (Synthroid, Levoxyl, Unithroid, Levothroid),
  • Armor Thyroid,
  • liothyronine (Cytomel).
  • Pia Levothyroxine pamoja na liothyronine huweza kupatikana kwenye kidonge kimoja(one tablet).

Dawa zote za tezi la shingoni(thyroid medications) unashauriwa kutumia tumbo likiwa halina kitu, lakini dawa jamii ya Levothyroxine, hii imeonekana zaidi kuingiliana na maziwa au bidhaa za maziwa hali ambayo inaathiri ufyonzwaji au kupelekea zifyozwe kwa kiwango kidogo sana mwilini.

2. Dawa jamii ya Antibiotics

Kuna antibiotics nyingi ambazo hazipaswi kutumiwa pamoja na Maziwa au bidhaa za maziwa kwa sababu kalsiamu katika Maziwa inaweza kupunguza kiasi cha dawa ambazo mwili wako unaweza kutumia.

Mfano wa dawa hizo ni pamoja na;

  • Dawa jamii ya Tetracycline,
  • minocycline
  • doxycycline.

Ili kuepuka kuingiliana, unashauriwa kutumia dawa kama vile tetracyclines angalau kabla ya saa moja ndipo utumie maziwa/bidhaa zenye maziwa au utumie dawa hizi masaa mawili baada ya kutumia maziwa au bidhaa za maziwa.

Dawa zingine ni jamii ya Fluoroquinolone, kama vile;

  •  ciprofloxacin (Cipro),
  • levofloxacin (Levaquin), and
  • Pamoja na moxifloxacin (Avelox).

Kama vile mwingiliano wa maziwa na tetracyclines, matokeo sawa hutokea na kwenye dawa jamii ya fluoroquinolones. Tena, hii ina maana kwamba maambukizi yako yanaweza yasitibiwe kwa ufanisi au kikamilifu. Hii inaweza kufanya vijidudu kuwa vigumu zaidi kutibu katika maambukizo yajayo.

Unashauriwa kutumia dawa jamii ya fluoroquinolones angalau kabla ya masaa mawili ndipo utumie maziwa/bidhaa zenye maziwa au utumie dawa hizi masaa manne baada ya kutumia maziwa au bidhaa za maziwa.

3. Virutubisho vyote vyenye madini chuma(Iron Supplements)

Baadhi ya watu hutumia virutubisho vyenye madini ya chuma kwa tatizo la upungufu wa damu(anemia), hali ambayo damu yako haina chembechembe nyekundu za damu za kutosha(red blood cells).

Mfano wa dawa hizo ni pamoja na;

  • Dawa za Fefol, vidonge vya kuongeza damu kwa Mjamzito
  • ferrous sulfate
  • Pamoja na ferrous gluconate.

Kalsiamu katika bidhaa za maziwa inaweza kuzuia mwili kunyonya madini chuma ya kutosha kutoka kwenye dawa zako. Ndiyo maana inapendekezwa subiri angalau saa 2 baada ya kula bidhaa za maziwa kabla ya kutumia kirutubisho chako cha madini ya chuma.

Uchunguzi unaonyesha kuwa madini chuma hutumika vizuri zaidi kwenye tumbo ambalo halina kitu kwa sababu yatafyonzwa vizuri kwa njia hiyo.

Wakati mwingine, virutubisho vyenye madini chuma husababisha athari zisizofurahisha, kama vile tumbo kuuma n.k. Katika kesi hiyo, ni vizuri kuchukua ziada na chakula kidogo, lakini hakikisha kuwa sio chakula chenye maziwa kwa sababu kalsiamu ndani yake inaweza kuingiliana.

4. Dawa za matatizo ya mifupa kama vile Osteoporosis Medication

Osteoporosis ni hali inayotokea kwa watu wazee, hasa wanawake, ambapo mifupa yao hukonda na kuwa tete au dhaifu sana. Hatari ya kuvunjika mfupa huongezeka ikiwa una tatizo la osteoporosis. Dawa zinazoitwa bisphosphonates zimewekwa ili kuimarisha mifupa.

Maziwa,bidhaa za maziwa au vyakula vyenye kiwango kikubwa cha Calcium huweza kuathiri ufyonzwaji wa dawa hizi, hali ambayo husababisha dawa hizi kufyozwa katika kiwango kidogo na hivyo kutumika katika kiwango kidogo zaidi mwilini.

Mfano wa dawa hizo ni pamoja na;

  • Actonel (risedronate),
  • Fosamax (alendronate),
  • Pamoja na Boniva (ibandronate).

Ikiwa unatumia dawa hizi, hakikisha unasubiri saa kadhaa kabla ya kunywa maziwa au kula bidhaa nyingine za maziwa,

Dawa kama vile Bisphosphonates kwa kawaida unashauriwa kutumia asubuhi kabla hujala chochote( tumbo likiwa halina kitu),

Ukiwa unatumia dawa za alendronate pamoja na risedronate, unahitaji kusubiri angalau dakika 30 baada ya kutumia dawa kabla ya kutumia bidhaa zozote za maziwa,

Na Ukiwa unatumia ibandronate za kunywa unahitaji kusubiri angalau dakika 60.

5. Dawa jamii ya Lithium

Dawa jamii ya Lithium salts hutumika kwa watu wenye matatizo kama vile bipolar disorder, matatizo yanayohusu afya ya akili(psychiatric illnesses) kama vile depression pamoja na schizophrenia.

Pia hushauriwi kuchanganya dawa hizi pamoja na maziwa au bidhaa za maziwa,

Ikiwa unatumia dawa hizi, hakikisha unasubiri saa kadhaa kabla ya kunywa maziwa au kula bidhaa nyingine za maziwa.

6. Dawa za Virusi vya Ukimwi(HIV Medication)

Moja ya dawa zinazotumika kwa wagonjwa wenye VVU ni pamoja na Dovato na Tivicay (dolutegravir),

dawa hizi hutumika zikiwa vimeunganishwa pamoja na dawa zingine za Ukimwi.

Na wakati mwingine dawa za dolutegravir hutumika kama kinga(prophylactic) ili kuzuia maambukizi kwa mtu ambaye amekuwa kwenye mazingira hatarishi ya kupata VVU.

Kutumia dolutegravir na virutubisho vya kalsiamu ni sawa ikiwa imechukuliwa pamoja na chakula. Vinginevyo, mwingiliano huu unaweza kusababisha ufyozwaji wa chini wa dawa hizi.

Kuchanganya vitu hivi viwili kunaweza kusababisha kupungua kwa viwango vya dawa kwenye damu, Inapendekezwa kuchukua dolutegravir masaa mawili kabla au saa sita baada ya kutumia vyakula au virutubishi vyenye kalsiamu.

Hitimisho:

Hizo ndyo baadhi ya Dawa ambazo haziruhusiwi kuchanganya na maziwa.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Dalili za infection kwenye damu Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia...

Magonjwa4 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa1 week ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa4 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa4 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa1 month ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Trending