Connect with us

Magonjwa

Kuota vipele kwenye mashavu ya uke

Avatar photo

Published

on

Kuota vipele kwenye mashavu ya uke

vipele kwenye mashavu ya uke huweza kusababishwa na sababu nyingi mbali mbali ikiwemo matatizo ya ngozi,maambukizi ya magonjwa n.k,

Na Dawa ya vipele kwenye mashavu ya uke hutegemea na chanzo husika cha tatizo hili. Katika Makala hii tunajadili Zaidi kuhusu tatizo la Kuota vipele kwenye mashavu ya uke, chanzo chake,dalili pamoja na Tiba yake.

Dalili za vipele kwenye mashavu ya uke

Kwa kawaida dalili za vipele kwenye mashavu ya uke huambatana na muwasho wa mara kwa mara, na hali hii ya muwasho huzidi kuongezeka au kuwa mbaya Zaidi pale unapojikuna eneo husika.

Kwa Ujumla dalili za vipele kwenye mashavu ya uke ni pamoja na;

  • Kupata muwasho au kuhisi kuungua sehemu ya upele kuota
  • Kutokea kwa vipele vinavyoonekana kwa macho
  • Kuwa na malengelenge au vidonda
  • Ngozi kuwa na mabaka mabaka
  • Kuvimba kwa ngozi
  • Wengine hupata homa

vipele kwenye mashavu ya uke huweza kuambatana pia na;

– Uchafu wenye harufu mbaya kutoka ukeni

– Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa n.k

Chanzo cha vipele kwenye mashavu ya uke

Asilimia kubwa tatizo la vipele kwenye mashavu ya uke ni tatizo ambalo hutibika na husababishwa na sababu za kawaida, Ingawa wakati mwingine huweza kuwa tatizo Sugu na ambalo halitibiki kulingana na chanzo chake.

Hizi hapa ni baadhi ya Sababu za vipele kwenye mashavu ya uke;

1. Matatizo ya Ngozi kama vile Contact dermatitis,

Tatizo hili la ngozi ni miongoni mwa matatizo yanayosababisha vipele kwenye mashavu ya uke kwa kiasi kikubwa.

Baadhi ya Tafiti za Mwaka 2014 zilionyesha Contact dermatitis huhusika na tatizo la vipele kwenye mashavu ya uke kwa karibu asilimia 50% ya wanawake wenye shida hii.

2. Tatizo la kuvimba kwa Uke au mashavu ya Uke(Vaginitis au vulvovaginitis),

kwa mujibu wa vituo vya kudhibiti na kuzuia magonjwa “the Centers for Disease Control (CDC)”, moja ya chanzo kikubwa cha tatizo hili ni maambukizi ya bacteria au fangasi.

3. Maambukizi ya Fangasi-Yeast infections (Candida),

Watu wengi wenye vipele kwenye mashavu ya uke pia hutokana na maambukizi ya fangasi sehemu za siri hasa fangasi ambao hujulikana kama Candida albicans.

4. Magonjwa ya Zinaa kama vile Trichomoniasis (trich),

ugonjwa huu hudababishwa na protozoan parasite na husambazwa kwa njia ya kujamiiana.

Tiba ya Trichomoniasis ni pamoja na matumizi ya antibiotics kama vile metronidazole (Flagyl) au tinidazole (Tindamax).

5. Tatizo la Psoriasis

Psoriasis ni tatizo kwenye mfumo wa kinga ya mwili(autoimmune condition) ambalo matokeo yake huathiri ngozi ikiwemo ngozi ya Sehemu za Siri.

Tatizo hili huweza kuwa chanzo cha vipele kwenye mashavu ya uke au vidonda(Psoriasis lesions),

Lakini tatizo hili la Psoriasis haliwezi kuathiri sehemu ya ndani ya Uke.

6. Maambukizi ya Virusi- Molluscum contagiosum

Molluscum contagiosum ni maambukizi ya Virusi ambayo kwa asilimia kubwa hushambulia ngozi, maambukizi haya huweza kusambaa kwa njia ya kujamiiana n.k,

Moja ya dalili zake ni kusababisha upele(bumps) wenye ukubwa wa millimeters kati ya 2 mpaka 5 (mm).

7. Ugonjwa wa Scabies

Moja ya dalili kubwa za ugonjwa wa Scabies ni kusababisha vipele kwenye ngozi ambavyo huweza kuambatana na muwasho,

Hivo wanawake wenye ugonjwa wa Scabies huwezs kupata tatizo la vipele kwenye mashavu ya uke.

8. Kuwa na Chawa Sehemu za Siri(Pubic lice)

Chawa Sehemu za siri(Pubic lice) ni wadudu jamii ya parasite wadogo sana ambao huweza kuathiri nywele za Sehemu za Siri na chakula chao kikubwa ni damu ya binadamu.

Unaweza kuwapata baada ya kujamiiana na mtu mwenye hawa chawa, au kupitia nguo,mashuka,taulo za kuogea n.k kutoka kwa mtu mwenye chawa.

Wadudu hawa huweza kusababisha hali ya muwasho sehemu za Siri na eneo la mashavu ya Uke kwa ujumla.

Chawa Sehemu za Siri(Pubic lice) huweza kutibiwa na dawa kama vile permethrin (Nix).

9. Maambukizi ya Genital herpes

Genital herpes husababishwa na Virusi vinavyojulikana kama herpes simplex virus, hasa hasa aina ya 2 (HSV-2).

Huu ni miongoni mwa magonjwa ya Zinaa yanayoenezwa kwa kiasi kikubwa, na asilimia kubwa dalili zake huchukua siku 4 mpaka 7 kuanza kuonekana toka siku ya kuambukizwa.

Dalili zake ni pamoja na kuwa na vipele, malengelenge au vidonda vyenye maumivu pamoja na kuhisi hali ya kuungua sehemu za Siri, kuzunguka uke, kwenye matako, na sehemu ya haja kubwa.

10. Ugonjwa wa Kaswende(Syphilis)

Kaswende ni ugonjwa wa zinaa ambao husababishwa na bacteria Treponema pallidum. Ugonjwa huu pia huweza kusababisha vipele kwenye mashavu ya uke au vidonda ambazo hujulikana kama chancre.

11. Tatizo la masundosundo(Genital warts)

Tatizo hili ni miongoni mwa magonjwa ya Zinaa ambapo chanzo chake ni maambukizi ya human papillomavirus (HPV).

Pia tatizo hili huweza kusababisha vipele kwenye mashavu ya uke.

Hizo ndyo baadhi ya Sababu za Mwanamke kupata Tatizo la vipele kwenye mashavu ya uke.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa2 days ago

kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani

kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani Unapopata tatizo la kuharisha na kutapika kwa wakati mmoja unaweza kuwaza sana,...

Magonjwa4 days ago

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Dalili za infection kwenye damu Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia...

Magonjwa7 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa2 weeks ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa4 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa4 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa1 month ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa1 month ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Trending