Ticker

6/recent/ticker-posts

Dalili za sickle cell kwa mtoto pamoja na matibabu yake



Dalili za sickle cell kwa mtoto

Katika Makala hii tunachambua Zaidi kuhusu Dalili za sickle cell kwa mtoto,chanzo cha ugonjwa wa Sickle cell pamoja na Matibabu yake.

Sickle cell ni nini?

Sickle cell ambapo kiswahili chake ni “Seli mundu” ni ugonjwa ambao upo kwenye kundi la inherited red blood cell disorders,

kwa kawaida seli nyekundu za damu(red blood cells) huwa na umbo linalojulikana kama biconcave disks, lakini Ugonjwa wa sickle cell husababisha umbo la seli nyekundu za damu kuwa kama ‘C’ yaani C-shaped au “sickle.” na hapa ndipo jina la ugonjwa huu kuitwa Sickle cell hutokea.(tazama shape kwenye picha)

kutokana na seli nyekundu za damu kuwa na shape au umbo lisilo la kawaida,hii hupelekea seli hizo kufa mapema zaidi,

Na hiki ndyo chanzo kikubwa cha wagonjwa wa Sickle cell kuwa na tatizo la Upungufu wa damu kila mara.

Hayo ndyo maelezo mafupi ya utangulizi kuhusu ugonjwa wa Sickle cell.

Aina za Ugonjwa wa Sickle cell

Kuna aina mbali mbali za ugonjwa wa sickle cell ikiwemo;

  • HbSS
  • HbSC
  • HbS beta-thalassemia
  • HbSD
  • HbSE
  • HbSO
  • HbAS n.k

Chanzo cha Ugonjwa wa Sickle cell

Sickle cell ni ugonjwa ambao mtoto huzaliwa nao, ugonjwa huu wa sickle Cell au Seli mundu hutokana na kurithi kwa genes mbili ambazo huleta shida,

Mtoto hupokea genes mbili,moja kutoka kwa baba,na nyingine kutoka kwa mama, ambazo husababisha(code) matatizo kwenye hemoglobin kisha kupelekea uzalishwaji wa hemoglobin zenye shida yaani abnormal hemoglobin,

Na hapo ndipo ugonjwa wa Sickle cell hutokea.

Jinsi ya Kugundua ugonjwa wa sickle cell

ugonjwa wa sickle cell huweza kugundulika kwa kufanya vipimo vya damu yaani simple blood test.

Dalili za sickle cell kwa mtoto

Dalili za ugonjwa wa sickle cell kwa Ujumla zinahusisha zile zote za Mtu ambaye kaishiwa damu au ana tatizo la ANEMIA kama vile;

– Kushindwa kupumua vizuri

– Kizunguzungu

– Maumivu ya kichwa

– Ubaridi katika viganja na miguuni

– Unjano katika macho na ngozi au jaundice

– Weupe katika viganja, na eneo la macho liitwalo conjuctiva, ulimi na midomo

– Maumivu ya tumbo

– Homa

– Maumivu ya viungo (joint pains)

– Maumivu ya kifua

– Damu katika mkojo (hematuria)

– maumivu ya mfupa

– kuziba kwa ateri kuu (CRAO) n.k

Matibabu ya Ugonjwa wa Sickle cell kwa Mtoto

Kwa mujibu wa chapisho la Vituo vya kudhibiti na kuzuia magonjwa yaani centers for diseases control and prevention(CDC)

Tiba pekee ya ugonjwa wa sickle cell ambayo huweza kutibu kabsa tatizo hili ni;

  • bone marrow transplant
  • Au stem cell transplant.

FAQs: Maswali ambayo huulizwa mara kwa mara

Je, ugonjwa wa seli mundu ni nini?

Seli mundu ni ugonjwa ambao upo kwenye kundi la inherited red blood cell disorders, ugonjwa huu kwa jina lingine hujulikana kama “Sickle cell”

kwa kawaida seli nyekundu za damu(red blood cells) huwa na umbo linalojulikana kama biconcave disks, lakini Ugonjwa wa seli mundu husababisha umbo la seli nyekundu za damu kuwa kama ‘C’ yaani C-shaped au “sickle.” na hapa ndipo jina la ugonjwa huu kuitwa Sickle cell hutokea.

Je, chanzo cha ugonjwa wa seli mundu ni kipi?

Seli mundu ni ugonjwa ambao mtoto kuzaliwa nao, ugonjwa wa Seli mundu hutokana na kurithi kwa genes mbili ambazo huleta shida,

Mtoto hupokea genes mbili,moja kutoka kwa baba,na nyingine kutoka kwa mama, ambazo husababisha(code) matatizo kwenye hemoglobin kisha kupelekea uzalishwaji wa hemoglobin zenye shida yaani abnormal hemoglobin,

Na hapo ndipo ugonjwa wa Seli mundu hutokea.

Hitimisho

Ni muhimu sana kufahamu kuhusu Dalili za Sickle cell kwa Mtoto ili kupata msaada kwa haraka zaidi,

Dalili za ugonjwa wa sickle cell au seli mundu kwa Ujumla zinahusisha zile zote za Mtu ambaye kaishiwa damu au ana tatizo la ANEMIA kama vile;

– Kushindwa kupumua vizuri

– Kizunguzungu

– Maumivu ya kichwa

– Ubaridi katika viganja na miguuni

– Unjano katika macho na ngozi au jaundice

– Weupe katika viganja, na eneo la macho liitwalo conjuctiva, ulimi na midomo

– Maumivu ya tumbo

– Homa

– Maumivu ya viungo (joint pains)

– Maumivu ya kifua

– Damu katika mkojo (hematuria)

– maumivu ya mfupa

– kuziba kwa ateri kuu (CRAO)

• Soma zaidi hapa kuhusu Ugonjwa wa Sickle cell(seli mundu)



Post a Comment

0 Comments