Ticker

6/recent/ticker-posts

Dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi(ARVs)



Dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi(ARVs)

ARVs ni kifupi cha neno antiretroviral drugs, ikiwa na maana ya dawa kwa ajili kupunguza makali ya Virusi vya Ukimwi,

Hivo basi ARV sio dawa moja bali ni kundi au mjumuisho wa dawa zote ambazo hutumika kwa Mgonjwa mwenye virusi vya Ukimwi(VVU) na mfano wa dawa hizo ni kama vile;

  •  Zidovudine
  • Tenofovir
  • Abacavir
  • Lamivudine
  • Didanosine
  • Emtricitabine n.k

Dawa za VVU zinaweza kusaidia kupunguza wingi wa virusi, kupambana na maambukizi, na kuboresha maisha yako. Zinaweza kupunguza uwezekano wa kusambaza VVU pia, lakini kama ukizitumia vibaya, bado unaweza kuwapa wengine VVU,

Kumbuka pia; Dawa hizi za ARVs Sio tiba ya kuondoa kabsa VVU.

>>Malengo ya dawa hizi ni:

  • Kudhibiti ukuaji wa virusi vya Ukimwi(VVU)
  • Kuboresha mfumo wako wa kinga ya mwili Kufanya kazi vizuri
  • Kupunguza Dalili au kuzuia kabsa dalili za Ukimwi kujitokeza
  • Kuzuia maambukizi ya VVU kwa wengine.n.k

Imeidhinishwa matumizi ya zaidi ya dazeni mbili za dawa za kurefusha maisha kwa ajili ya maambukizi ya VVU. Mara nyingi dawa hizi(ARVs) hugawanywa katika makundi sita kwa sababu hufanya kazi kwa njia tofauti. Madaktari wanapendekeza kuchukua mchanganyiko au “cocktail” ya angalau dawa kwenye makundi mawili. Hii inaitwa tiba ya kurefusha maisha, au antiretroviral therapy(ART).

Daktari wako atakujulisha hasa jinsi unapaswa kutumia dawa zako kwa usahihi. Unahitaji kufuata maagizo haswa, na haupaswi kukosa hata dozi moja. Ukikosa dozi, unaweza kupata aina za VVU zinazokinzana na dawa, na dawa zako zinaweza kuacha kufanya kazi.

Dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi(ARVs)

Haya ni baadhi ya makundi ambapo dawa za ARVs zimegawanywa;

1. Nucleoside/Nucleotide Reverse Transcriptase Inhibitors (NRTIs)

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  • Abacavir, or ABC (Ziagen)
  • Emtricitabine, or FTC (Emtriva)
  • Lamivudine, or 3TC (Epivir)
  • Tenofovir alafenamide, or TAF (Vemlidy)
  • Tenofovir disoproxil fumarate, or TDF (Viread)
  • Zidovudine or ZDV (Retrovir)

2.Non-nucleoside Reverse Transcriptase Inhibitors (NNRTIs)

Hapa kuna dawa kama vile;

  • Doravirine, or DOR (Pifeltro)
  • Efavirenz or EFV (Sustiva)
  • Etravirine or ETR (Intelence)
  • Nevirapine or NVP (Viramune)
  • Rilpivirine or RPV (Edurant)

3.Protease Inhibitors (PIs)

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  • Atazanavir or ATV (Reyataz)
  • Darunavir or DRV (Prezista)
  • Lopinavir + ritonavir, or LPV/r (Kaletra)
  • Ritonavir or RTV (Norvir)

4. Integrase Inhibitors

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  • Bictegravir or BIC (combined with other drugs as Biktarvy)
  • Cabotegravir and rilpivirine (Cabenuva)
  • Dolutegravir or DTG (Tivicay)
  • Elvitegravir or EVG (Vitekta)
  • Raltegravir or RAL (Isentress)

5.Fusion Inhibitors

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  • Enfuvirtide, or ENF or T-20 (Fuzeon)

6.Capsid Inhibitor

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  •  Lenacapavir(Sunlenca) n.k

Kumbuka; Dawa hizi hutumii moja peke yake zinakuwa kwenye mchanganyiko wa zaidi ya dawa moja(combination) Mfano;

Atazanavir + cobicistat, or ATV/c (Evotaz)
Darunavir + cobicistat, or DRV/c (Prezcobix)
Elvitegravir + TDF + FTC + cobicistat, or EVG/c/TDF/FTC (Stribild)
Elvitegravir + TAF + FTC + cobicistat, or EVG/c/TAF/FTC (Genvoya)

Bictegravir + tenofovir alafenamide + emtricitabine, or BIC/TAF/FTC (Biktarvy)
Dolutegravir + abacavir + lamivudine, or DTG/ABC/3TC (Triumeq)
Dolutegravir + rilpivirine, or DTG/RPV (Juluca)
Dolutegravir  + lamivudine, or DTG/3TC (Dovato)
Elvitegravir + cobicistat +  tenofovir alafenamide + emtricitabine, or EVG/c/TAF/FTC (Genvoya)
Elvitegravir + cobicistat + tenofovir disoproxil fumarate + emtricitabine, or EVG/c/TDF/FTC (Stribild)

Atazanavir + cobicistat, or ATV/c (Evotaz)
Darunavir + cobicistat, or DRV/c (Prezcobix)
Darunavir + cobicistat + tenofovir alafenamide + emtricitabine, or DRV/c/TAF/FTC) (Symtuza)
Non-nucleoside reverse transcriptase inhibitor (NNRTI)-based:

Doravirine + tenofovir disoproxil fumarate + lamivudine, or DOR/TDF/3TC (Delstrigo)
Efavirenz + tenofovir disoproxil fumarate + emtricitabine, or EFV/TDF/FTC (Atripla)
Rilpivirine + tenofovir alafenamide + emtricitabine , or RPV/TAF/FTC (Odefsey)
Rilpivirine + tenofovir disoproxil fumarate + emtricitabine, or RPV/TDF/FTC (Complera)

Abacavir + lamivudine, or ABC/3TC (Epzicom)
Abacavir + lamivudine + zidovudine, or ABC/3TC/ZDV (Trizivir)
Tenofovir alafenamide + emtricitabine, or TAF/FTC (Descovy)
Tenofovir disoproxil fumarate + emtricitabine, or TDF/FTC (Truvada)
Tenofovir disoproxil fumarate + lamivudine, or TDF/3TC (Cimduo)
Zidovudine + Lamivudine or ZDV/3TC (Combivir) N.K

>> Soma pia hapa kuhusu Muda sahihi wa Kutumia dawa za ARVs

>> Tofauti ya ARVs na PEP

Kuna PEP,PrEP,ARVS

Dawa za Kurefusha maisha(ARVs);

Dawa hizi sio za kutibu au kuponyesha kabsa Ukimwi bali hufanya kazi ya kupunguza Virusi vya ukimwi (Viral Load) hali ambayo huupa nafasi Mfumo wa kinga ya mwili kupambana vizuri na maambukizi haya.

Ili dawa hizi zilete matokeo mazuri unashauriwa kutokuacha kutumia dawa kutokana na maelekezo uliyopewa, kwani ni hatari na unaweza kutengeneza hali ya virusi kutokusikia dawa yaani Drug resistance.

Je ni Muda gani wa kuanza dawa za ARVs baada ya kugundulika una HIV?

Zipo Dhana mbali mbali kwenye jamii kuhusu Muda wa Kuanza dawa za ARVs baada ya kugundulika una Virusi vya UKIMWI,

Huku baadhi ya watu wakisema,hutakiwi kuanza dawa za ARVs mpaka uanze kuumwa, je ni kweli?

Soma zaidi hapa chini…!!!

Tiba ya VVU inahusisha unywaji wa dawa zenye ufanisi mkubwa yaani antiretroviral therapy (ART) ambazo hufanya kazi kudhibiti virusi.

ART inapendekezwa kwa kila mtu mwenye VVU.

Watu walio na VVU wanapaswa kuanza ART haraka iwezekanavyo baada ya utambuzi (hata siku hiyo hiyo).

Nimatumaini yangu kwamba umepata majibu kuhusu Muda wa kuanza dawa za kufubaza Virusi vya Ukimwi maarufu kama ARVs.



Post a Comment

0 Comments