Ticker

6/recent/ticker-posts

Mwanajeshi AARON aliyejichoma moto afariki Dunia



Mwanajeshi AARON aliyejichoma moto afariki Dunia

Mwanajeshi wa Jeshi la Anga la Marekani Aaron Bushnell mwenye umri wa miaka 25 ambaye alijirekodi video akipinga vita dhidi ya Wapalestina, amefariki dunia saa chache baada ya kujichoma moto nje ya Ubalozi wa Israel uliopo Washington DC Nchini Marekani.

Japo Maofisa wa usalama waliokua karibu na eneo la tukio walifanya jitihada za kumuokoa kwa kuuzima moto huo muda mfupi baadae, imeonekana tayari Aaron alikua amejeruhiwa kwa kiasi kikubwa kwani majeraha aliyoyapata ndio yaliyosababisha kifo chake leo.

Aaron ambaye anatokea San Antonio, Texas alisikika akisema maneno yafuatayo kwenye video aliyojirekodi “Sitashiriki tena katika mauaji ya halaiki, nitashiriki katika kitendo cha kupinga kilichokithiri, Palestina huru (ikomboe Palestina!), sehemu ya video hiyo ipo kwenye slide ya pili.

Tukio hili la Aaron limekuja wakati maandamano yakiongezeka nchini Marekani kupinga vita ya Israel dhidi ya Palestina.



Post a Comment

0 Comments