Ticker

6/recent/ticker-posts

Mwanasoka wa Ivory Coast, Archange Defrignan Mondou afariki dunia



Mwanasoka wa Ivory Coast, Archange Defrignan Mondou afariki dunia.

Mchezaji kandanda wa Ivory Coast Archange Defrignan Mondou, umri miaka 19, amefariki dunia baada ya mwili wake kupatikana nyumbani kwake bila kujua chanzo cha kifo chake ni nini.

Mondou, 19, alichezea klabu kuu ya Norway HamKam huko Eliteserien kabla ya kifo chake.

Kiungo huyo aliyepewa jina la utani Achilles, alihama kutoka Ivory Coast Aprili mwaka jana na awali alijiunga na kikosi cha pili cha HamKam, akicheza mechi tatu na kufunga bao moja.

Mondou alipatikana katika nyumba yake huko Hamar, maili 60 kaskazini mwa mji mkuu wa Norway Oslo Jumanne, Februari 27. Sababu ya kifo chake haifahamiki mpaka Sasa..!!!!

Katika taarifa, HamKam ilisema: ‘Ni kwa huzuni kubwa kwamba HamKam Football imepokea taarifa kwamba Achilles ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 19.

‘Alipatikana katika nyumba yake. Katika kipindi hiki kigumu tupo pamoja na familia yake na jamaa.

Sababu ya kifo haijajulikana.’

Meneja mkuu wa HamKam Bent Svele aliongeza: ‘Hii ni siku ngumu sana kwa kila mtu aliyeguswa.’

Wakati huo huo, polisi wa eneo hilo walisema chanzo cha kifo cha Mondou hadi sasa hakijajulikana.

Walieleza: ‘Alipatikana amekufa, na tumeomba uchunguzi wa maiti.

“Hakukuwa na chochote cha kutilia shaka juu ya kifo hicho, zaidi ya kusema sababu haijulikani. Alipatikana na wengine nyumbani, na akafa peke yake.’

Mondou alilazimika kujitenga na soka Septemba mwaka jana kufuatia tukio lililotekea mazoezini, huku kiungo huyo akitumia muda hospitalini baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu.



Post a Comment

0 Comments