Ticker

6/recent/ticker-posts

TANZIA:Ali Hassan mwinyi afariki dunia



TANZIA:Ali Hassan mwinyi afariki dunia,

Raisi Mstaafu awamu ya Pili Mzee Ali Hasani mwinyi afariki Dunia.

Rais wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi afariki dunia leo Alhamisi Februari 29,2024. Tangazo la kifo chake Limetolewa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Rais wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 98.

Mzee Ally Hassan Mwinyi amefariki Dunia leo Februry 29,2024 saa 11:30 jioni Hospitalini Jijini Dar es salaam alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa saratani ya mapafu.

Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza msiba huo leo ambapo amesema Mzee Mwinyi ambaye alikuwa Rais kuanzia mwaka 1985 hadi 1995, amekuwa akipatiwa matibabu tangu November 2023 London Uingereza na baadaye kurejea Nchini na kuendelea na matibabu Jijini Dar es salaam.

Rais Samia ametangaza siku saba za maombolezo kuanzia kesho kufuatia kifo hicho.

Ali Hassan Mwinyi (8 Mei 1925-29 February 2024) alikuwa Rais wa pili wa Tanzania kuanzia mwaka 1985 hadi 1995.

Aliyemtangulia ni Mwalimu Julius Nyerere, na aliyemfuata ni Benjamin Mkapa. Pia alikuwa mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuanzia mwaka 1990 hadi 1996.

Ali Hassan Mwinyi alizaliwa Mei 8, 1925 Kivure mkoani Pwani. Alikuwa rais wa pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia 1985 – 1995. Aliwahi pia kuwa rais wa Zanzibar, makamu wa rais na waziri wa Mambo ya ndani.



Post a Comment

0 Comments