Connect with us

Magonjwa

Saratani ya Mapafu: Chanzo, Dalili, na Mbinu za Tiba

Avatar photo

Published

on

Saratani ya Mapafu: Chanzo, Dalili, na Mbinu za Tiba

Saratani ya Mapafu ni ugonjwa ambao huhusisha ukuaji wa seli usiowakawaida(abnormal/uncontrolled cell growth) kwenye eneo la Mapafu.

Saratani ya mapafu ni mojawapo ya magonjwa yanayosumbua jamii duniani kote, na inaweza kusababisha madhara makubwa kwa afya ya binadamu,

Kuelewa chanzo, dalili, na njia za kutibu saratani hii ni muhimu sana katika mapambano dhidi ya ugonjwa huu ambao huweza kusababisha Kifo.

Chanzo cha Saratani ya Mapafu

Uvutaji wa sigara ni sababu kuu inayohusishwa na saratani ya mapafu,

Kemikali zinazopatikana kwenye moshi wa sigara, kama vile nikotini na tar, zinaweza kusababisha mabadiliko katika seli za mapafu na kusababisha ukuaji usio wa kawaida wa seli, ambao hatimaye unaweza kuwa saratani.

Hata hivyo, ni muhimu kuelewa kuwa wale wasiovuta sigara pia wanaweza kuwa katika hatari ya kupata saratani ya mapafu kutokana na kuwa kwenye mazingira yenye moshi wa sigara.

Vitu hivi huweza kuongeza hatari ya Mtu kupata Saratani ya Mapafu;

– Uvutaji wa Sigara, kama nilivyoelezea hapo juu

– Wasiovuta sigara pia wanaweza kuwa katika hatari ya kupata saratani ya mapafu kutokana na kuwa kwenye mazingira yenye moshi wa sigara.

– Kupata huduma ya Mionzi hapo kabla(Previous radiation therapy),

Ikiwa umepitia matibabu ya mionzi kwenye kifua kwa aina nyingine ya saratani, unaweza kuwa na hatari kubwa ya kupata saratani ya mapafu.

– kuwepo kwenye Mazingira yenye gesi aina ya radon gas,

Radoni huzalishwa na mgawanyiko wa asili wa uranium katika udongo, miamba na maji ambayo hatimaye huwa sehemu ya hewa unayopumua. Viwango visivyo salama vya radoni vinaweza kujilimbikiza katika jengo lolote, pamoja na nyumba,

Hali hii huongeza hatari ya wewe kupata Saratani ya Mapafu.

– Kuwepo kwenye mazingira yenye asbestos pamoja na carcinogens nyingine, mfano; arsenic, chromium pamoja na nickel —inaweza kuongeza hatari ya kupata saratani ya mapafu, hasa ikiwa wewe ni mvutaji sigara.

– Kuwa na Historia ya Saratani ya Mapafu kwenye familia yako(Family history of lung cancer),

Watu walio na mzazi, ndugu au mtoto aliye na saratani ya mapafu wana hatari kubwa ya kupata ugonjwa huu.

Dalili za Saratani ya Mapafu

Saratani ya mapafu kwa kawaida haisababishi dalili katika hatua zake za awali. Ishara na dalili za saratani ya mapafu kawaida hutokea wakati ugonjwa unapoendelea,

Dalili za saratani ya mapafu zinaweza kutofautiana, lakini baadhi ya dalili kuu ni pamoja na;

  1. kukohoa kwa muda mrefu,
  2. Kupata maumivu ya kifua,
  3. kutoa damu kwenye Makohozi,
  4. Kupata shida ya kupumua au kubana pumzi,
  5. kupoteza uzito kwa ghafla
  6. Na wengine hupata maumivu ya kichwa pamoja na Mifupa.

Ni muhimu kufahamu dalili hizi na kushauriana na wataalamu wa afya ikiwa zinaonekana.

Uchunguzi na Utambuzi:

Utambuzi wa saratani ya mapafu mara nyingi hufanywa kupitia uchunguzi wa picha kama vile;

  • X-ray,
  • CT-Scan
  • au uchunguzi wa MRI.

Mara tu saratani inapogundulika, hatua zaidi za uchunguzi zinaweza kufanyika kujua hatua na kubaini njia bora za matibabu.

Matibabu ya Saratani ya Mapafu

Mbinu za Tiba juu ya Saratani ya Mapafu:

Matibabu ya saratani ya mapafu hutegemea hatua ya ugonjwa wakati wa utambuzi,

Kwa hatua za awali, upasuaji wa kuondoa tumor unaweza kuwa chaguo. Hatua za juu zaidi zinaweza kuhitaji matibabu ya mionzi au kemotherapy. Mbinu hizi zinaweza kutumika pekee au kwa pamoja kulingana na hali ya mgonjwa.

Mapambano Dhidi ya Saratani ya Mapafu:

Kuzuia saratani ya mapafu kunahusisha kuepuka uvutaji wa sigara na kujiepusha na mazingira yenye moshi wa sigara,

Watu wanapaswa kuchukua hatua za kufanya uchunguzi wa mara kwa mara, haswa wale walio katika vikundi vya hatari.

Kubadilisha tabia za maisha, kama vile kufuata lishe bora na kudumisha afya njema, pia ni muhimu katika mapambano dhidi ya saratani hii inayoweza kuzuilika.

Hitimisho:

Saratani ya mapafu ni tishio kubwa kwa afya ya umma, na kuelewa chanzo chake, dalili, na njia za kutibu ni muhimu. Elimu na ufahamu juu ya athari za uvutaji sigara na mazingira yenye moshi wa sigara ni hatua muhimu kuelekea jamii yenye afya.

Kupitia jitihada za pamoja za kuzuia, kutambua mapema, na kutibu, inawezekana kupunguza CASES za saratani ya mapafu na kuhakikisha afya bora kwa wote.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Ushauri|Tiba|CheckIn 🩺🌡️ContactUs; +255758286584 or INBOX📩. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...