Connect with us

Magonjwa

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Avatar photo

Published

on

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam hujulikana kama Dysuria (Painful Urination)

Dysuria inamaanisha unahisi maumivu au hisia ya kuungua wakati unapokojoa (kukojoa). Wanaume na wanawake wa umri wowote wanaweza kupata dysuria, lakini ni kawaida zaidi kwa wanawake.

Maambukizi ya mfumo wa mkojo(UTI) mara nyingi huhusishwa na dysuria, Matibabu ya hali hii ya kuumia wakati wa kukojoa hutegemea na sababu au chanzo chake.

Mkojo kuuma au Dysuria sio ugonjwa bali ni dalili ya tatizo au ugonjwa flani, na mara nyingi hali hii huambatana na hali ya kukojoa mara kwa mara.

Nani anaweza kupata shida hii ya Mkojo kuuma au Dysuria

Wanaume na wanawake wa umri wowote wanaweza kupata shida hii ya mkojo kuuma, Ingawa hali hii Ni kawaida zaidi kwa wanawake. Maambukizi ya mfumo wa mkojo (UTIs) mara nyingi huhusishwa na dysuria. UTI hutokea kwa wanawake zaidi kuliko kwa wanaume.

Watu wengine walio katika hatari kubwa ya kupata shida ya Mkojo kuuma au dysuria ni pamoja na:

  • Wanawake wajawazito.
  • Wanaume na wanawake wenye ugonjwa wa kisukari.
  • Wanaume na wanawake wenye aina yoyote ya ugonjwa wa kibofu.

Chanzo cha Mkojo kuuma ni nini?

Sababu Zinazowezekana tumezigawanya kulingana na jinsia ya mtu, kama ifuatavyo;

WANAWAKE: Kukojoa kwa uchungu kwa wanawake kunaweza kuwa matokeo ya:

– Maambukizi ya kibofu (cystitis).

– Maambukizi ya uke

– Maambukizi ya njia ya mkojo au UTI

– Tatizo la Endometritis na sababu nyingine nje ya maambukizi kwenye njia ya mkojo, ikiwa ni pamoja na tatizo la diverticulosis na diverticulitis.

– Kuvimba kwa kibofu cha mkojo au urethra (urethritis) (Urethra ni mrija unaoanzia sehemu ya chini ya kibofu chako na kutoka nje ya mwili wako),

Kuvimba kwa kawaida husababishwa na maambukizi.
Kuvimba kunaweza pia kusababishwa na kujamiiana, matumizi ya douchi, baadhi ya sabuni,Toilet paper, sponji za kuzuia mimba au dawa za kuua manii.n.k.

WANAUME: Kukojoa kwa uchungu kwa wanaume kunaweza kuwa ni matokeo ya:

+ Maambukizi ya mfumo wa mkojo(UTI) na maambukizi mengine nje ya njia ya mkojo, ikiwa ni pamoja na diverticulosis na diverticulitis.

– Ugonjwa wa Saratani ya Tezi dume(Prostate cancer)

NB; Pia Mkojo kuuma kwa wanaume na wanawake kunaweza kuwa ni matokeo ya magonjwa ya zinaa (STIs) au athari ya dawa. Dawa za saratani au chemotherapy au matibabu ya mionzi kwenye eneo la fupanyonga huweza kusababisha kuvimba kwa kibofu cha mkojo na kusababisha kukojoa kwa maumivu.

Vipimo vya Kufanya ili kugundua Ugonjwa

  1. Kuchukua historia ya mgonjwa,ikiwemo kujua kama una historia ya magonjwa kama kisukari, upungufu wowote wa Kinga mwili n.k
  2. Kipimo cha Mkojo
  3. Kipimo cha magonjwa ya Zinaa n.k

Matibabu ya Mkojo Kuuma

Matibabu ya dysuria yanategemea sababu ya maumivu yako / hisia ya kuungua wakati wa kukojoa. Hatua ya kwanza katika matibabu yako ni kubaini kama kukojoa kwako kwa uchungu kunasababishwa na maambukizi, kuvimba, vipengele vya lishe, au tatizo la kibofu chako cha Mkojo.

Maambukizi ya mfumo wa mkojo(UTI) mara nyingi hutibiwa na dawa jamii ya antibiotics

Pia Zingatia baadhi ya Mambo muhimu kama vile;

  • Hakikisha unakunywa maji ya kutosha
  • Hakikisha usafi wako binafsi,ikiwemo nguo za ndani,vyoo n.k
  • Jikinge na magonjwa ya Zinaa(STDs) n.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa2 days ago

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Dalili za infection kwenye damu Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia...

Magonjwa4 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa1 week ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa4 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa4 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa1 month ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Trending