Magonjwa
kisukari aina ya pili,chanzo,dalili na Matibabu yake
kisukari aina ya pili,chanzo,dalili na Matibabu yake
Fahamu kuhusu kisukari aina ya pili,chanzo,dalili na Matibabu yake,Kupitia kwenye Makala hii hapa.
kisukari aina ya pili
kisukari aina ya pili(Type 2 diabetes) hutokea pale ambapo kuna shida kwenye jinsi mwili wako unavyorekebisha kiwango cha Sukari na kukitumia, ambapo matokeo yake ni uwepo wa kiwango kikubwa cha Sukari kwenye damu.
Dalili za kisukari aina ya pili
Dalili za kisukari aina ya pili(type 2 diabetes) mara nyingi hutokea taratibu, na unaweza kuishi na kisukari aina ya pili kwa miaka kadhaa bila hata kujua,
Ingawa pale ambapo dalili za kisukari aina ya pili zinapojitokeza,Moja ya dalili hizo ni pamoja na;
– Kiu kuongezeka Sana
– Kukojoa mara kwa mara
– Kuhisi njaa kila wakati
– Uzito kupungua kwa kasi sana
– Mwili kuchoka kupita kiasi
– Pale unapopata vidonda,Vidonda huchukua muda mrefu kupona au kwa Lugha nyingine vidonda hupona taratibu sana
– Kuona marue rue au kupata shida ya kuona
– Kupata maambukizi ya magonjwa mara kwa mara
– Kuhisi hali ya kuchoma, kuungua au GANZI kwenye mikono au miguu
– Kuwa na Eneo la ngozi lenye weusi zaidi,na mara nyingi hutokea kwapani na shingoni. N.k
Hizo ndyo baadhi ya Dalili za kisukari aina ya pili.
Chanzo cha kisukari aina ya pili
kisukari aina ya pili(type 2 diabetes) husababishwa na Sababu kuu Mbili,
- Kongosho( pancrease) kushindwa kuzalisha Kiwango cha kutosha cha insulin
- Seli za mwili kutoa matokeo hasi(respond poorly) dhidi ya insulin, pamoja na kutumia kiwango kidogo cha Sukari.
Vyote hivi Matokeo yake ni kuongezeka au kuwa na kiwango kikubwa zaidi cha Sukari Kwenye Damu.
Vitu ambavyo huongeza hatari ya mtu kupata kisukari aina ya pili
Vitu hivi hapa huweza kuongeza hatari ya kupata kisukari aina ya pili;
1. kuwa na tatizo la Uzito mkubwa au unene(overweight/obesity)
2. Kuwa na mafuta mengi mwilini(Fat distribution), hasa pale ambapo kiwango kikubwa cha mafuta kimehifadhiwa tumboni au kwenye eneo la abdomen badala ya kwenye hips pamoja na mapajani,
Hii huongeza hatari Zaidi ya kupata kisukari aina ya pili(type 2 diabetes).
3. Kutokufanya mazoezi,
Unashauriwa kufanya mazoezi angalau dakika 30 kila siku ili kupunguza hatari ya kupata magonjwa mbali mbali ikiwemo kisukari aina ya pili(type 2 diabetes)
4. Kukaa kwa muda mrefu Zaidi,
Kama kazi zako ni za kukaa kwa muda mrefu Zaidi,unashauriwa kila baada ya nusu saa ufanye angalau body movement kwa dakika kadhaa.
5. Family history, upo kwenye hatari ya kupata kisukari aina ya pili(type 2 diabetes) kama una Ndugu au wazazi wenye tatizo hili ndani ya familia yako
6. Umri, kadri umri unavyokuwa mkubwa zaidi ndivyo hatari ya kupata kisukari aina ya pili huongezeka zaidi,
hasa kwa watu wenye umri wa zaidi ya miaka 35 na kuendelea
7. Matatizo wakati wa Ujauzito, hatari ya kupata kisukari aina ya pili(type 2 diabetes) huongezeka kwa wanawake ambao wana historia ya kupata Kisukari wakati wa ujauzito yaani “gestational diabetes”.
8. Kuwa na tatizo la Polycystic ovary syndrome(PCOS).
Tatizo hili huweza kusababisha;
- mwanamke kupata hedhi bila mpangilio-irregular menstrual periods,
- nywele kukua au kuongezeka kupita kiasi mwilini
- Tatizo la obesity — ambalo huongeza hatari ya kupata kisukari aina ya pili(type 2 diabetes).
Matibabu ya kisukari aina ya pili
Hakuna tiba ya moja kwa moja ya kutibu kabsa kisukari aina ya pili(There’s no cure for type 2 diabetes),
Ila unaweza kudhibiti kiwango cha Sukari kwa kufanya haya;
âś“ Kupunguza Uzito kama una shida ya Uzito mkubwa
âś“ Kula vizuri vyakula bora na salama kwa afya
âś“ Kuepuka matumizi ya pombe kupita kiasi pamoja na Uvutaji wa Sigara ikiwemo tumbaku
âś“ kufanya mazoezi ya mwili
âś“ Kama hata baada ya kufanya na kuzingatia hivo,bado kiwango cha sukari kwenye damu hakishuki,
Dhibiti Sukari kwa kutumia dawa au matibabu ya Sukari kama vile
- Kutumia dawa za Sukari(diabetes medications
- Au kupata insulin therapy
FAQs: Maswali ambayo huulizwa mara kwa mara
Je, kisukari aina ya pili(type 2 diabetes) husababishwa na nini?
kisukari aina ya pili(type 2 diabetes) husababishwa na Sababu kuu Mbili,
- Kongosho( pancreas) kushindwa kuzalisha Kiwango cha kutosha cha insulin
- Seli za mwili kutoa matokeo hasi(respond poorly) dhidi ya insulin, pamoja na kutumia kiwango kidogo cha Sukari.
Vyote hivi Matokeo yake ni kuongezeka au kuwa na kiwango kikubwa zaidi cha Sukari Kwenye Damu.
Hitimisho
Zipo dali mbali mbali za kisukari aina ya pili(type 2 diabetes), na dalili hizo ni pamoja na;
– Kiu kuongezeka Sana
– Kukojoa mara kwa mara
– Kuhisi njaa kila wakati
– Uzito kupungua kwa kasi sana
– Mwili kuchoka kupita kiasi
– Pale unapopata vidonda,Vidonda huchukua muda mrefu kupona au kwa Lugha nyingine vidonda hupona taratibu sana
– Kuona marue rue au kupata shida ya kuona
– Kupata maambukizi ya magonjwa mara kwa mara
– Kuhisi hali ya kuchoma, kuungua au GANZI kwenye mikono au miguu
– Kuwa na Eneo la ngozi lenye weusi zaidi,na mara nyingi hutokea kwapani na shingoni. N.k
Ukiona dalili kama hizo hakikisha unapata msaada zaidi,hivo nenda hosptal kwa ajili ya kufanya Vipimo.
Hata hivo,Zipo njia mbali mbali za kupunguza hatari ya mtu kupata kisukari aina ya pili(type 2 diabetes), Na njia hizo ni pamoja na; Kufanya mazoezi ya mwili kila siku,kula vyakula bora kwa afya,kupunguza uzito wa mwili,Kuepuka matumizi ya Pombe kupita kiasi,Kuepuka Uvutaji wa Sigara n.k
Kwa kufanya hivo unaweza kupunguza kwa kiwango kikubwa hatari ya kupata kisukari aina ya pili(type 2 diabetes).
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.