Ticker

6/recent/ticker-posts

Una dalili zote za COVID-19 lakini ukipima hauna Ugonjwa



Una dalili zote za COVID-19 lakini ukipima hauna Ugonjwa.

JN.1, lahaja kuu kwa sasa ya COVID-19 inayochangia takriban asilimia 86% ya aina zote zinazozunguka za SARS-CoV-2, inaweza kuchukua muda mrefu kuonyesha matokeo chanya kwenye kipimo cha COVID ambacho watu wengi hujipima wakiwa nyumbani hasa kwenye nchi kama Marekani(home antigen tests),

Hali hii hupelekea watu wengi wana Dalili Zote za COVID-19 lakini wakifanya vipimo ugonjwa hauonekani.

Baadhi ya Wataalam wa afya pamoja na wagonjwa wamekuwa wakiripoti kwamba; Vipimo walivyofanya siku kadhaa baada ya dalili kujitokeza vilileta majibu NEGATIVE, Kisha baada ya siku Zaidi hapo baadae majibu yakawa POSITIVE. (link Source)

Soma Zaidi hapa; hali ilivyo kwa Sasa kuhusu ugonjwa wa COVID-19

Hii inasababisha kuwa na wasiwasi juu ya ubora wa Vipimo. “Je, vipimo vya nyumbani(home-antigen tests) vinaweza kugundua JN.1?” alitweet mtumiaji mmoja kwenye mtandao wa X, ambayo zamani ulijulikana kama Twitter, akionyesha pia wasiwasi wa wengine kwenye mitandao ya kijamii.

Kabla ya kulaumu Vipimo kwa kupoteza ufanisi — au lahaja hii ya COVID(JN.1) kuwa vigumu kugunduliwa — wataalam wa magonjwa ya kuambukiza hutoa ufafanuzi mwingine;

mifumo yetu ya kinga ni imara kuliko-2020. Pia wanaelekeza kwenye utafiti uliochapishwa mnamo Septemba ambao uligundua wagonjwa wengi hawapati majibu CHANYA kwenye kipimo hadi siku 4 baada ya kuambukizwa.

Mifumo yetu ya kinga inazidi kuimarika, alisema Peter Chin-Hong, MD, mtaalamu wa magonjwa ya kuambukiza na profesa wa dawa katika Chuo Kikuu cha California, San Francisco, Shule ya Tiba.

Wakati janga hilo likiendelea na idadi kubwa ya watu wamepata maambukizo, chanjo, au zote mbili, “Ni muhimu kuchukua tahadhari. Anaendelea kwa kusema..!!!

Hiyo inamaanisha kuwa tunaweza kugundua wagonjwa mapema wenye COVID kwa hivi sasa ikilinganishwa na hapo awali kwenye janga hili.



Post a Comment

0 Comments