Connect with us

Magonjwa

Dalili za ugonjwa wa covid 19,Chanzo na Matibabu yake

Avatar photo

Published

on

Dalili za ugonjwa wa covid 19,Chanzo na Matibabu yake

 UGONJWA WA COVID19 NI NINI?

Huu ni ugonjwa wa kuambukiza ambao umesababishwa na kirusi aina mpya cha corona, Ugonjwa huu wa covid 19 ulianzia jiji la Wuhan, nchini China mwezi Disemba 2019.

JE UGONJWA WA COVID19 UNASAMBAA VIPI?

Ugonjwa wa covid 19 huweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja hadi mtu mwingine kupitia vitone vidogo vidogo vya mate vinavyoruka toka puani au mdomoni pale mtu mwenye maambukizi ya virusi vya Corona anapopiga chafya , kukohoa au kupumua.

Vitone hivi vya mate huweza kutua kwenye nyuso za watu au vitu, watu wengine hupata virusi hivi wanapogusa hivi vitu,

Vitone hivi vikiruka hewani mtu anapopiga chafya au kukohoa mtu mwingine huweza kuvivuta ndani na hewa anapopumua, hivyo ni muhimu kukaa umbali wa mita 1 kutoka kwa mtu anayeumwa ili kujikinga na ugonjwa wa covid 19.

DALILI ZA UGONJWA WA COVID19 NI ZIPI?

Dalili za ugonjwa wa COVID19 kwa wagonjwa wengi ni pamoja na;

  • homa,
  • uchovu
  • Pamoja na kikohozi kikavu.

Wagonjwa wengine hupata dalili kama;

  • misuli kuuma,
  • pua kubana,
  • mafua kutiririka,
  • maumivu ya koo
  • au kuharisha.

Dalili hizi huwa ni ndogo na huanza taratibu.

Endelea Zaidi hapa kusoma Dalili za ugonjwa wa covid 19,

DALILI ZA ugonjwa wa covid 19,

1. Mgonjwa, joto la mwili kupanda au kupata homa

2. Mgonjwa kupata maumivu makali ya kifua wakati wa kukohoa

3. Mgonjwa kubanwa na mbavu

4. Mgonjwa kupatwa na Mafua makali yanayoambatana na kichwa kuuma sana

5. Mgonjwa kupata Kikohozi kikavu

6. Mgonjwa kupata uchovu wa mwili kupita kiasi

7. Mgonjwa kushindwa kupumua au kupata shida wakati wa kupumua

8. Mgonjwa kupoteza hamu ya kula

9. Wakati mwingine Mgonjwa kuharisha( Nadra) n.k

UCHUNGUZI WA ugonjwa wa covid 19,

Moja ya vitu ambavyo huchunguzwa ni pamoja na joto la Mwili, mate au sampuli za Damu za mtu ambaye anaonyesha dalili hizi za ugonjwa wa covid 19.

NJIA ZA KUJIKINGA NA ugonjwa wa covid 19,

1. Nawa vizuri mikono yako kwa sabuni na maji safi

2. Epuka kukaa maeneo yenye Msongamano wa watu wengi

3. Funika mdomo wako kwa kutumia masks au maarufu kama Barakoa

4. Epuka kuwa karibu au kugusana na mtu mwenye dalili

5. Epuka kusalimia watu kwa kuwashika Mikono

JE UNAWEZA VIPI KUJIKINGA NA MAAMBUKIZI YA UGONJWA WA COVID19

– Nawa mikono mara kwa mara kwa maji tiririka na sabuni au kutumia dawa maalumu ya kuua wadudu (Hand sanitizer)

Kwa nini? Ukinawa mikono kwa sabuni na maji au kutumia dawa maalumu ya kusafisha mikono utaondoa virusi ambao hukaa kwenye mikono mara nyingi,

Hii ni moja ya Njia muhimu sana ya kujikinga na ugonjwa wa covid 19.

– Jiweke mbali zaidi ya mita moja kutoka kwa mtu anayekohoa au kupiga chafya,

Kwa nini? Mtu anapopiga chafya au kukohoa hurusha vitone au chembechembe za mate ambazo huweza kuwa zimebeba virusi. Ukiwa karibu sana utawavuta virusi hawa unapovuta hewa kupumua.

– Acha kushikashika macho, pua na mdomo kwa mikono ambayo hujaisafisha

Kwa nini? Mikono hugusa sehemu mbalimbali hivyo huweza kubeba virusi. Unapogusa macho ,pua au mdomo virusi hupata njia ya kuingia mwilini na kukufanya upate ugonjwa wa covid 19.

– Iwapo unaumwa mafua, homa au shida ya kupumua usiendelee na shughuri zako nenda hospitali

Kwa nini? Vituo vya huduma ya afya vina taaarifa zote kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa covid 19 pia huweza kukupatia tiba sahihi kuhusu tatizo lako pia hukulinda na kusaidia usisambaze maambukizi kwa watu wengine.

– Kutokushikana mikono au kukumbatiana, hii pia ni mojawapo ya njia za kukukinga dhidi ya ugonjwa wa covid 19.

FAQs: Maswali yanayoulizwa mara kwa mara

Je, kuepuka kushikana mikono inaweza kusaidia kukukinga na ugonjwa wa covid 19,

Ndyo, Moja ya Njia ya kukukinga na ugonjwa wa covid 19, ni pamoja na kuepuka kushikana mikono.

Hitimisho

Ugonjwa wa covid 19, ni miongoni mwa magonjwa ya mlipuko ambayo yamesababisha Vifo Vingi Zaidi duniani,

Unaweza kujikinga na ugonjwa wa covid 19 kwa kutumia Njia hizi;Hakikisha unapata chanjo ya Kuzuia ugonjwa wa covid 19,Nawa mikono kila mara kwa maji Safi tiririka pamoja na sabuni,

Epuka kukaa maeneo yenye Msongamano wa watu wengi,Funika mdomo wako kwa kutumia masks au maarufu kama Barakoa hasa unapokuwa sehemu za watu wengi, Epuka kuwa karibu au kugusana na mtu mwenye dalili za ugonjwa wa Covid 19,Epuka kusalimia watu kwa kuwashika Mikono n.k

Ukiona dalili Zozote ambazo huzielewi hakikisha unawahi hospital kwa ajili ya uchunguzi Zaidi,

Kwa Kuzingatia njia hizi unaweza kujikinga na Ugonjwa wa Covid 19.

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa6 days ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa3 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa4 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa4 weeks ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Magonjwa1 month ago

Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga

“Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga” Kifo cha ghafla ni janga lisilotarajiwa ambalo linaweza kumpata...

Trending