Connect with us

magonjwa ya wanawake

Nini kinasababisha hedhi kuchelewa

Avatar photo

Published

on

Nini kinasababisha hedhi kuchelewa

Endapo una aina ya mzunguko wa hedhi ambao haubadiliki badiliki yaani regular menstrual cycles, kuna wakati unaweza kukutana na vipindi vya hedhi kuchelewa kuliko kawaida,

Hii huweza kukupa wasi wasi nini kinaendelea mwilini, Moja ya Sababu ya haraka haraka ambayo unaweza kufikiria ni kuhusu kubeba Mimba.

Katika Makala ya Leo,tumechambua Sababu kuu zinazoweza kukusababishia Hedhi yako ichelewe.

Nini kinasababisha hedhi kuchelewa

Zipo Sababu nyingi ambazo huweza kuchangia tatizo hili, na Baadhi ya Sababu hizo ni pamoja na;

1. Kufanya Mazoezi kupita kiasi, Exercising Rigorously

Kila kitu kinataka kiasi, hata Mazoezi tunasema yana Faida nyingi mwilini lakini pia yanataka Kiasi,

Unaweza kuona shida ya kuchelewa kwa hedhi kutokana na kufanya mazoezi mazito. Mazoezi ya nguvu ya mara kwa mara yanaweza kusababisha vipindi visivyo kawaida vya hedhi ikiwemo kukosa hedhi. Unaweza pia kupata hedhi isiyo ya kawaida ikiwa utaanza kufanya mazoezi tena baada ya kutofanya kwa muda.

Mazoezi kupita kiasi husababisha physical stress mwilini mwako, Hali ambayo huuambia Ubongo Kuacha kuzalisha vichocheo yaani reproductive hormones.

Moja ya vichocheo hivo ni Pamoja na gonadotropin-releasing hormone (GnRH).  Hormone hii ndyo inayohusika na Muda wa Hedhi yako kutoka,Ikiwa Ubongo haujaitoa au unaitoa Taratibu sana hedhi inaweza kuacha Kutoka.

2.  Mabadiliko kwenye Uzito wa Mwili

Kichocheo cha Estrogen kwa asilimia kubwa huzalishwa kutoka kwenye tishu zinazotengeneza mafuta baada ya kipindi cha Ukomo wa Hedhi(menopause),tishu hizi hufahamika kama adipose tissue,

Ingawa,Mwanamke mwenye mafuta yaliyozidi,mwili wake huweza kuzalisha estrogen nyingi kipindi chochote cha Maisha yake sio tena baada ya kufikia ukomo wa hedhi. Hii ina maana kadri kiwango cha Mafuta kinapozidi mwilini ndivo kiwango cha estrogen huongezeka pia.

Matokeo yake,Estrogen ikizidi huathiri mzunguko wa hedhi na kuleta madhara kama vile;

  • Kuvuja damu nyingi ya Hedhi
  • Kukosa Hedhi
  • Hedhi kuchelewa kutoka
  • Au Hedhi kutokutoka kwa mpangilio

Hivo ukiwa na Uzito Mkubwa upo kwenye hatari hii,

FAHAMU,Kama Uzito wako wa mwili unapungua kupita kiasi kwa kasi sana upo kwenye hatari ya Kupata mabadiliko ya Hedhi Pia.

Estrojeni ni muhimu kwa ajili ya kujenga ukuta wa uterasi kwa mimba inayoweza kutokea wakati wa mzunguko wa hedhi. Unapopoteza uzito mwingi, mwili wako hautoi estrojeni ya kutosha.

3. Kuwa na Msongo wa Mawazo au Stress

Hali ya Stress inaweza kusababisha mabadiliko ya Hedhi ikiwemo hedhi kuchelewa kutoka,

Utafiti umeonyesha kuwa watu walio na viwango vya juu vya mfadhaiko,Msongo wa mawazo au Stress pia walikuwa wakipata vipindi visivyo kawaida vya HEDHI.

Wakati STRESS inaathiri muda wa hedhi, inaweza kuathiri uzazi Pia. Wale ambao wana Stress kwa kiwango kikubwa wanaweza kuwa na wakati mgumu zaidi wa kupata mimba au kuwa na ujauzito usio na matatizo.

4. Mabadiliko ya vichocheo au Hormones mwilini

Mfano kwenye tezi la thyroid—Homoni za tezi la Thyroid huwajibika kwa udhibiti wa nishati ya mwili wako na huathiri viungo vingi. Viwango vya homoni za tezi hili vinapokuwa juu au chini, utendaji wa mwili wako unaweza kubadilika—pamoja na utendajikazi wako wa mzunguko wa hedhi.

Kwa wale wanaozalisha kiwango kikubwa cha thyroid hormone— huweza kupata Hedhi karibu karibu , Na wale ambao hawazalishi thyroid hormone ya kutosha huweza kupata hedhi kwa kuchelewa au mara chache Zaidi

5. Kuwa kwenye Mazingira yenye Dawa za kuua wadudu,Exposure to Pesticides

Pesticides zinaweza kuwa na uhusiano wa karibu na mabadiliko ya Hedhi yaani irregular periods.

Washiriki wa utafiti mmoja walikuwa wamekabiliwa na dawa za kuulia wadudu kutokana na kufanya kazi kwenye mashamba, kuishi ndani yake, au vyote viwili.

Wengi walikabiliwa na viuatilifu vya kemikali vinavyovuruga mfumo wa endocrine, dawa ya kuua wadudu inayojulikana kusababisha mabadiliko ya hedhi. Washiriki waliripoti hitilafu katika urefu wa mzunguko wao na kutokuwepo kwa kipindi chao cha Hedhi kwa zaidi ya siku 90.

6. Unyonyeshaji

Ukichagua kunyonyesha mara kwa mara, kipindi chako cha Hedhi hakirudi mara moja. Hii inajulikana kama Lactational amenorrhea, Na hutokea baada ya mtu kujifungua na huongeza muda wa mtu kupata mimba tena. Kwa sababu hiyo, baadhi ya watu huitumia kama njia ya uzazi wa Mpango.

7. Umri

Kipindi chako cha Hedhi kinaweza kisiwe cha kueleweka hadi miaka yako inapofikia 20. Hata hivyo, unapokaribia kukoma hedhi, hedhi inaweza kuwa isiyo ya kawaida tena.

Ingawa labda unatarajia kupata Hedhi kidogo unapokaribia kukoma kwa hedhi, inaweza kutofautiana kulingana na wakati wake. Kwa mfano, hedhi yako inaweza kusimama kwa miezi michache kisha kurudi bila kutarajia.

Hizo ndyo baadhi ya Sababu za Kuchelewa kwa Hedhi…!!!!

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILINE KWA NAMBA +255758286584.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa4 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa8 hours ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa4 days ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa3 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa3 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa4 weeks ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa4 weeks ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Magonjwa1 month ago

Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga

“Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga” Kifo cha ghafla ni janga lisilotarajiwa ambalo linaweza kumpata...

Trending