Connect with us

Magonjwa

Jinsi Ya Kukabiliana Na Tatizo La Kuvurugika Mzunguko Wa Hedhi

Avatar photo

Published

on

Jinsi Ya Kukabiliana Na Tatizo La Kuvurugika Mzunguko Wa Hedhi

TATIZO la kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi huwakumba wanawake wengi waliopo kwenye umri wa kuzaa au wale wanaokaribia kufikia ukomo wa hedhi.

Japokuwa wengine huchukulia tatizo hili kama kitu cha kawaida, kuvurugika kwa hedhi ni dalili kwamba kuna tatizo katika mfumo wako wa uzazi hivyo ni lazima uchukue hatua za haraka za kubaini tatizo hilo.

Kabla hatujaangalia tatizo lenyewe, ni vizuri tukatazama jinsi mzunguko wa kawaida wa mwanamke unavyotakiwa kuwa. Siku ya kwanza unayoona damu ya hedhi, kitaalamu ndiyo siku ya kwanza katika mzunguko wako.

Wapo wanawake wenye mzunguko mfupi na wapo wengine wenye mzunguko mrefu, wastani ukiwa ni siku 28. Hata hivyo, kitaalamu, mzunguko wa kawaida unajumuisha kuanzia wale wanaochukua siku 21 kukamilisha mzunguko mpaka wale wanaotumia siku 35.

Jambo la msingi la kuelewa ni kwamba urefu au ufupi wa mzunguko wako siyo tatizo, tatizo linakuja pale siku zinapopishana bila sababu ya msingi. Kwamba mwezi huu mzunguko wako umechukua siku 28, lakini mwezi unaofuata unachukua siku 32 na mwezi mwingine unaofuata unachukua siku 24.

Hapo ndipo penye tatizo, lakini hata kama mzunguko wako ni wa siku 32 lakini kila mwezi tarehe zinacheza hapohapo, basi hauna tatizo.

Wapo ambao wakati mwingine wanavusha hata mwezi mmoja au miwili bila kuona siku zao wakati hawana ujauzito, kama na wewe upo kwenye kundi hili basi tambua kwamba una tatizo ambalo ni lazima lishughulikiwe mapema.

CHANZO CHA TATIZO

Tatizo hili huweza kusababishwa na kuvurugika kwa mfumo wa homoni mwilini, hasa homoni au vichocheo vinavyoendesha na kudhibiti hedhi na uzazi kwa jumla.

Uwepo wa uvimbe ndani ya kizazi au kwenye vifuko vya mayai pia ni tatizo. Mabadiliko katika tabaka la ndani la kizazi, maambukizi sugu ya kizazi na kuharibika kwa mimba ni mojawapo ya matatizo haya yanayochangia siku za hedhi zitoke bila ya mpangilio.

Matumizi ya baadhi ya madawa huweza kuvuruga homoni na kusababisha matatizo haya.

DALILI ZA TATIZO

Mwanamke mwenye tatizo hili hulalamika kutofahamu mwenendo wa mzunguko wake, hulalamika damu kutoka muda mrefu au siku chache sana chini ya siku tatu, wakati mwingine hapati kabisa.

Anaweza kuwa na maumivu ya tumbo chini ya kitovu, maumivu wakati wa hedhi, maumivu wakati wa kujamiiana na hata damu kutoka mabonge au nyingi na nyepesi. Pia ataelezea ni muda mrefu anatafuta mtoto lakini hapati.

UCHUNGUZI

Tatizo hili humuathiri mwanamke kwa kiasi kikubwa hasa pale damu inapotoka kwa muda mrefu kwa zaidi ya siku saba au asipopata kabisa hedhi katika umri wake kama unamruhusu, pia mwanamke hatakuwa vizuri anapopata maumivu wakati wa hedhi, au anapotafuta mtoto halafu hapati ujauzito.

Uchunguzi hufanyika katika kliniki za madaktari bingwa wa akina mama katika hospitali za mikoa, vipimo mbalimbali vitafanyika kadiri daktari atakavyoona inafaa. Vipimo pia vitazingatia mahitaji ya mwanamke kama yupo tayari kushika ujauzito kwa kipindi hicho. Kwa hiyo katika upimaji atachunguzwa na mfumo wake wa uzazi.

NINI CHA KUFANYA?

Ni vema mwanamke mwenye matatizo haya akazingatia ushauri wa daktari wake ili aweze kupona na kufanikiwa malengo yake ya kupata ujauzito. Baada ya uchunguzi wa kina ndipo utaratibu wa matibabu unaanza.

Mwanamke ambaye ameshafikia ukomo wa kuzaa yaani zaidi ya miaka arobaini na tano na ana matatizo haya basi azingatie sana uchunguzi na tiba.

Pamoja na kwamba tumeona vyanzo mbalimbali vya tatizo hili, lakini pia tusisahau saratani au kansa ya shingo ya kizazi, kwa ujumla vinabidi vichunguzwe kwani dalili zake hazitofautiani sana na matatizo mengine. Wahi hospitali kwa uchunguzi na tiba.

Karibu AfyaUpdates Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In https://afyaclass.com  Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Dalili za infection kwenye damu Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia...

Magonjwa4 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa1 week ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa4 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa4 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa1 month ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Trending