Connect with us

News

TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani

Avatar photo

Published

on

Mfanyabiashara maarufu na aliyekuwa mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, Yusuf Manji amefariki dunia Jumamosi Juni 29, 2024 saa 6 usiku katika Jimbo la Florida nchini Marekani alipokuwa anapatiwa matibabu.

Manji (49), ambaye alifariki dunia saa sita usiku akiwa miezi miwili iliyopita alifanya mahojiano marefu na gazeti hili ambapo alizungumza mambo mengi kuhusiana na soka, hususani timu za Yanga na Simba.

Mtoto wa marehemu, Mehabub Manji alilithibitishia Mwananchi kuhusu kifo cha baba yake akisema alianza kuugua ghafla na kwenda hospitali sehemu ambayo umauti ulimkuta.

“Ukweli ni kwamba baba amefariki hapa Florida, Marekani. Nafikiri taarifa nyingine nitakupa baadaye,” alisema Mehabub ambaye alikuwa akiongozana na baba yake mara kwa mara walipokuwa jijini Dar es Salaam na kwenye mechi za Yanga kwa Mkapa.

Mwenyekiti huyo wa zamani ambaye alichukua ubingwa wa Ligi Kuu Bara mara nne 2012/2013 na mara tatu mfululizo 2014/2015, 2015/2016 na 2016/2017.

Pia, alifanikiwa kutwaa Ngao ya Jamii, Kombe la Shirikisho FA na Kombe la Kagame 2012 likiwa ndiyo kombe la mwisho la michuano hiyo kwa Yanga.

Akiwa na Yanga kipindi chote timu ilifuzu Ligi ya Mabingwa Afrika ingawa haikufanya vizuri sana, anakumbukwa na mashabiki wa timu hiyo kama mmoja kati ya viongozi wenye mafanikio makubwa zaidi Jangwani lakini akiwa mmoja kati ya watu walioleta mapinduzi ya soka Tanzania.

Manji ambaye aliingia madarakani siku chache baada ya Yanga kuchapwa mabao 5-0 na Simba kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara, Mei 6, 2012 alifanya kazi kubwa kipindi cha uongozi ikiwamo kuhakikisha anavunja makundi mawili makubwa yaliyokuwa yanapingana ndani ya timu hiyo moja likiitwa Yanga Asili na lingine Yanga Kampuni.

Manji aliiongoza Yanga kwa miaka mitano akiingia madarakani 2012 na kujiuzulu 2017 baada ya kukwaruzana na wazee wa timu hiyo akiwemo marehemu Yahaya Akilimali, anakumbukwa na wana Yanga kwa kufanikiwa kuwasajili wachezaji wakubwa kama Juma Kaseja, Kelvin Yondani, Mbuyu Twite, Emannuel Okwi, Thaabani Kamusoko, Obrey Chirwa na Donald Ngoma kwenye kikosi chake.

Mbali na wachezaji mahiri ambao walisajiliwa, Manji pia aliajiri makocha kadhaa wakubwa wakiwemo Konstadian Papic, Milutin Sredojevic Micho, Sam Timbe, Ernest Brandts, Marcio Maximo, George Lwandamina na Tom Santifiet na kuleta mabadiliko makubwa katika soka la Tanzania.

Mfanyabiashara huyo ambaye alijiuzulu uenyekiti Yanga, Mei 21, 2017 katika mahojiano yake ya hivi karibuni na gazeti hili alisema anaamini Simba kwa sasa inashindwa kufanya vizuri baada ya kufariki dunia kwa aliyekuwa mwenyekiti wa kamati ya usajili ya timu hiyo, Zacharia Hans Pope ambaye aliamini alikuwa na ubora wa hali ya juu kutambua wachezaji mahiri sokoni.

“Simba ni timu kubwa Tanzania, ina fanbase kubwa sana lakini mimi naamini kuwa inashuka kwa sasa kwa kuwa mtu mmoja muhimu sana hayupo. Ukitazama utagundua kuwa Simba imeanza kushuka tangu alipofariki Zacharia Hans Pope, huyu alikuwa mtu wa tofauti sana lakini alikuwa anajua ni mchezaji gani anatakiwa kwa kipindi gani.

“Pamoja na kwamba alikuwa na timu yake na mimi yangu, lakini tulikuwa marafiki wakubwa na mara kwa mara tulikuwa tukikutana tunazungumza kama ndugu bila kuweka Usimba na Uyanga wetu,” ilikuwa kauli ya mwisho ya Manji alipofanya mahojiano maalumu na Mwananchi Dijital.

Hata hivyo, katika mahojiano hayo Manji alisema alifanikiwa kutazama  michezo miwili ya Yanga ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Mamelodi Sundowns na mchezaji wake mahiri kuliko wote aliyemuona kwenye kikosi cha Yanga ni Stephen Aziz Ki.

 “Nilifanikiwa kuutazama mchezo ule wa Yanga kule Afrika Kusini dhidi ya Mamelodi ambao Yanga ilifungwa kwa penalti, niliwaona wamecheza vizuri sana, lakini kuna mchezaji mmoja nilimuona ana nywele za Blonde (blichi), alionyesha kiwango cha juu sana na nimemuona pia kwenye mechi ya Dabi.

“Sijamfahamu vizuri jina lake, unajua siku hizi siyo kama zamani, sasa navaa miwani na umri umeenda,” Alipoonyeshwa picha tofauti za wachezaji wa Yanga alipomuona Aziz Ki alisema:“ Huyohuyo ndiye ninamaanisha huku akicheka, anakwenda uwanjani akijua nini anakwenda kufanya, ndiye ananivutia sana akiwa na Yanga nafikiri kila mmoja atakubaliana nami.”

Mara baada ya Manji kujiuzulu klabu hiyo ilipita kwenye ukata mkubwa ambapo ilianza kutembeza bakuli kwa ajili ya kujiendesha ambapo lilipewa jina la Kubwa Kuliko na kuhamishia utawala wa soka la Tanzania kwa Simba ambayo ilitwaa ubingwa wa ligi mara nne mfululizo na Azam mara moja, hadi timu hiyo ilipopata uwekezaji wa GSM ndiyo ikarejea kwenye makali yake ya kutwaa ubingwa mara tatu mfululizo hadi msimu uliopita.

Wasifu wa Hayati Yusuf Manji

Alizaliwa Oktoba 14, 1975 katika Jiji la Dar es Salaam, Tanzania

Mwaka 1995 alianzisha kampuni ya Quality Group Limited iliyofahamika Tanzania na Afrika kwa kusambaza bidhaa mbalimbali.

Alisoma shahada ya uhasibu kutoka Chuo cha Hofstra kilichopo jiji la New York, Marekani.

Mwaka 2015, alichaguliwa kuwa Diwani wa Mbagala Kuu kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)

Enzi za uhai wake, Manji alifanikiwa kupata watoto wawili

Aliiongoza Yanga kwa miaka mitano akiingia madarakani 2012 na kujiuzulu 2017

Anakumbukwa na Wana Yanga kwa kutwaa mataji manne ya ligi kuu, Ngao ya Jamii na Kombe la Kagame na kuwasajili wachezaji wakubwa kama Kelvin Yondani, Juma Kaseja na Emannuel Okwi na wengine wengi.

Amefariki dunia Juni 29, 2024 Jimbo la Florida nchini Marekani alipokuwa akipatiwa matibabu.

Manji amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 49.

Via:Mwananchi

Karibu AfyaUpdates Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In https://afyaclass.com  Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa2 days ago

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Dalili za infection kwenye damu Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia...

Magonjwa4 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa1 week ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa4 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa4 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa1 month ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Trending