Connect with us

Magonjwa

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Avatar photo

Published

on

Dalili za infection kwenye damu

Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba

Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia lakini maana yake ni “maambukizi kwenye damu-blood infection”

Endapo damu yako imepimwa na kuonekana ina viini vya magonjwa kama vile bacteria n.k utaambiwa damu yako ni Chafu au una tatizo la mchafuko wa damu.

Maambukizi kwenye damu kwa Lugha nyingine tunaita Blood Infection au kwa kitaalam Zaidi wanatumia neno “Sepsis”

Sepsis ni nini?

Sepsis ni pale ambapo mwili wako unakuwa na mwitikio mkali dhidi ya maambukizi kwenye damu. Wakati huo mfumo wako wa kinga, ambao kwa kawaida unakukinga dhidi ya vijidudu, huanza kushambulia tishu za mwili wako.

Hii husababisha uvimbe unaoweza kusababisha uharibifu wa viungo. Pia ni kawaida kwa mabonge ya damu kuundwa hali ambayo hupunguza mtiririko wa damu kwenye viungo vyako vya ndani, na kusababisha visipate virutubisho na oksijeni inayohitajika.

Mchafuko wa damu huhusisha kuwa na vimelea vya magonjwa kwenye damu, vimelea hivo ni pamoja na;

  • Bacteria(asilimia kubwa)
  • Fangasi
  • Virusi
  • Parasites

Chanzo cha Mchafuko wa damu

Kama tulivyosema, haya ni maambukizi ya viini vya magonjwa kwenye damu, viini hivi ni pamoja na bacteria, parasites, fangasi au viruses.

Unaweza kupata maambukizi kwenye damu kwa njia mbali mbali ikiwemo;

  • Kupitia IV lines kama upo hospitalini,
  • Kwenye vidonda
  • Kupitia mpira ya mkojo(urinary catheters)
  • vyakula unavyokula ikiwemo nyama n.k

Maambukizi haya huweza kupelekea tatizo la Sepsis;

– Pneumonia

– UTI-Urinary tract infections

– maambukizi kwenye kidole tumbo-appendix (appendicitis)

– Maambukizi tumboni(Abdominal infection)

– Maambukizi kwenye Ini au kifuko cha nyongo

– Maambukizi kwenye Ubongo au Uti wa mgongo

Aina ya Bacteria wanaosababisha mchafuko wa damu

Aina ya Bacteria wanaosababisha kwa kiasi kikubwa mchafuko wa Damu(Sepsis) ni pamoja na;

  • Staphylococcus aureus (S. aureus),
  • Streptococcus pyogenes (S. pyogenes),
  • Klebsiella spp.,
  • Escherichia coli (E. coli),
  • Pamoja na Pseudomonas aeruginosa (P. aeruginosa)

Watu ambapo wapo kwenye hatari ya kupata Mchafuko wa Damu

Watu ambapo wapo kwenye hatari ya kupata mchafuko wa damu ni pamoja na;

• Wenye kinga dhaifu ya Mwili

• Wenye magonjwa kama vile;

• Wajawazito

• Ambao wameshawahi kupata tatizo la mchafuko wa damu hapo kabla

• Wenye umri wa Zaidi ya miaka 65, hasa hasa ikiwa wana matatizo mengine ya kiafya

• Waliowahi kulazwa hospital kwa kuugua sana muda mrefu au kufanyiwa Upasuaji

• Wanaotumia mpira wa mkojo(Urinary cathers) au mipira ya kupumulia(breathing tubes)

• Wenye Vidonda vikubwa, kuungua au kupata majeraha mbali mbali kwenye ngozi

Dalili za Mchafuko wa damu

Hizi hapa ni baadhi ya dalili za mchafuko wa damu;

1. Kuwa na Homa

2. Mwili kutetemeka sana

3. kupata shida ya kukosa pumzi au kupumua kwa shida

4. Kuwa na dalili kama za kuchanganyikiwa

5. Joto la mwili kushuka sana

6. Kukojoa kidogo sana kuliko kawaida au kutokukojoa kabsa.

7. Mapigo ya Moyo kwenda mbio

8. Kuhisi kichefuchefu na kutapika

9. Kupata tatizo la Kuharisha

10. Mwili kuchoka sana, kuwa dhaifu au kukosa nguvu

11. Kutoa sana jasho

12. Kupata maumivu makali ikiwemo ya kichwa n.k

13. Kupata upele kwenye ngozi(Skin rashes)

14. Kuhisi kizunguzungu

15. Kuhisi usingizi sana

16. Ngozi kuwasha sana n.k

Ukiona dalili hizi hakikisha unapata Msaada Mapema au;

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa4 hours ago

kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani

kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani Unapopata tatizo la kuharisha na kutapika kwa wakati mmoja unaweza kuwaza sana,...

Magonjwa2 days ago

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Dalili za infection kwenye damu Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia...

Magonjwa5 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa1 week ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa4 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa4 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa1 month ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Trending