Connect with us

Uzazi/Ujauzito

Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji

Doctor Ombeni

Published

on

63 Views
0 Comments

Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji

Baada ya kufanyiwa Upasuaji wa kujifungua kwa kitaalam Cesarean Section(C-Section), Moja ya vitu muhimu vya kuzingatia ni hali ya kidonda chako,

Unashauriwa kukitunza kidonda kwa uangalifu ili kisipate Maambukizi yoyote(infections), na Ukiona Dalili hizi hakikisha unapata Msaada mapema;

1. Kuvimba eneo la kidonda ulipofanyiwa upasuaji

2. Kidonda kuanza kuvuja maji maji

3. Kidonda kuvuja Damu

4. Kupata maumivu makali sana ya kidonda ambayo hayaishi hata baada ya kutumia dawa

5. Sehemu ya Kidonda kubadilika rangi na kuwa nyekundu Sana(Redness around the incision)

6. Kidonda kutoa harufu mbaya n.k

Vitu ambavyo huongeza hatari ya kupata madhara wakati wa kujifungua kwa Upasuaji

Ingawa ni mara chache sana kutokea,ila vitu hivi huweza kuchangia madhara;

– Mtoto kuwa Mkubwa Sana

– Mama kuwa Mnene kupita kiasi

– Kuwa na Labor ya Muda mrefu Zaidi

– Kuwa na Mzio au Allergies na dawa za USINGIZI

– Damu yako kuwa ndogo Sana

– Kuwa na magonjwa kama vile Kisukari n.k

#SOMA hapa kwanini Wanawake wengi hujifungua kwa Upasuaji?

Madhara ya Kujifungua kwa Upasuaji(Complications)

Haya ni baadhi ya madhara ambayo huweza kutokea baada ya kujifungua kwa Upasuaji;

• Maambukizi ya kidonda

• Kupata homa

• Kupoteza damu nyingi

• Kupata majeraha kwa baadhi ya viungo(organs)

• Hali ya Dhararua inayopelekea utolewe kabsa kizazi(emergency hysterectomy)

• Kupata madhara kutokana na kuwa na allergy au mzio na dawa za Usingizi

• Mtoto kudhurika wakati wa Upasuaji

• Mama kupoteza Maisha N.k

Kwa bahati nzuri, matatizo makubwa kutokana na kujifungua kwa upasuaji ni nadra sana kutokea. Katika nchi zilizoendelea, vifo vinavyotokana na uzazi ni nadra sana kutokea.

Na Mara nyingi vifo havihusiani na kitendo cha Upasuaji bali vinahusiana na matatizo ya ujauzito ambayo hukufanya kuzaa kwa upasuaji.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

63 Views
0 Comments

Medical Disclaimer

Medical Disclaimer: Taarifa kwenye makala hii ni kwa ajili ya Updates au elimu ya jumla tu na haichukui nafasi ya uchunguzi,Tiba au ushauri wa kitaalamu wa daktari kwa mtu mmoja mmoja. Kama una dharura au tatizo lolote la kiafya, tafadhali Wasiliana na Daktari moja kwa moja hapa.

Je, unahitaji ushauri binafsi au matibabu ya tatizo lolote?

💬 Wasiliana na Daktari Hapa

🏆Certified| Doctor from Afyaclass. Maudhui haya ni kwa ajili ya elimu ya jumla ya afya. Unapohitaji ushauri wa kina, uchunguzi, au matibabu binafsi, wasiliana na daktari kupitia namba:+255758286584.Pia tufwatilie kupitia: @Facebook | @Instagram | @YouTube.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Guest Avatar

LATEST POSTS

Uzazi/Ujauzito4 hours ago

Mama mjamzito akiwa na mimba ya miezi 8 anaruhusiwa kusafiri safari ndefu ya masaa zaidi ya 24?

Mama mjamzito akiwa na mimba ya miezi 8 anaruhusiwa kusafiri safari ndefu ya masaa zaidi ya 24? Ndiyo, mama mwenye...

EVENTS5 hours ago

Siku ya Usalama wa Mgonjwa Duniani 2026: Huduma Salama kwa Magonjwa Yasiyoambukiza

Siku ya Usalama wa Mgonjwa Duniani (World Patient Safety Day) huadhimishwa kila mwaka tarehe 17 Septemba kwa lengo la kuongeza...

Hospital23 hours ago

MNH-Mloganzila Yafanya Upasuaji wa Kurekebisha na Kurefusha Mifupa kwa Mbinu ya Ilizarov

MNH-Mloganzila Yafanya Upasuaji wa Kurekebisha na Kurefusha Mifupa kwa Mbinu ya Ilizarov Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)-Mloganzila imefanikiwa kufanya kwa...

EVENTS1 day ago

Wavunja Record ya Dunia kwa kupanda miche 2,51,446 kwa saa moja tu

Wavunja Record ya Dunia kwa kupanda miche 2,51,446 kwa saa moja tu. Katika juhudi kubwa za kushangaza kwenye kutunza mazingira,...

magonjwa ya wanawake1 day ago

Fangasi Ukeni: Chanzo na Dalili

Fangasi Ukeni: Chanzo na Dalili Fangasi ukeni ni maambukizi ya fangasi yanayotokea kwenye uke na mara nyingi husababishwa na fangasi...

magonjwa ya wanawake2 days ago

Hedhi yenye harufu mbaya: SABABU zinazoweza kusababisha

Kwa baadhi ya wanawake, damu ya hedhi inaweza kuwa na harufu fulani ambayo si sawa na harufu ya kawaida ya...

EVENTS2 days ago

Siku ya kuzuia kujiua duniani 2026: kubadili mtazamo na kuanza mazungumzo

SIKU YA KUZUIA KUJIUA DUNIANI 2026: KUBADILI MTAZAMO NA KUANZA MAZUNGUMZO Kaulimbiu ya 2026: “Changing the Narrative on Suicide” –...

Utafiti2 days ago

Vifo Vinavyotokana na Mimba kutunga Nje ya Kizazi

Mimba kutunga nje ya kizazi (ectopic pregnancy) ni hali ambayo mimba inajipandikiza nje ya sehemu ya kawaida ya kizazi,Mara nyingi...

Utafiti2 days ago

Ucheleweshaji wa huduma Ndani ya Hospitali Wawa Tishio Kubwa kwa Maisha ya Mama na Mtoto

Ucheleweshaji wa huduma ndani ya vituo vya afya umeonekana kuwa moja ya sababu kubwa zinazochangia vifo vya wajawazito na watoto...

Afya News3 days ago

Jinsi Dawa za Kulevya Zinavyoharibu Afya ya Kinywa na Meno

Matumizi ya dawa za kulevya yanaweza kuathiri sehemu mbalimbali za mwili, ikiwemo ubongo, moyo, ini na mfumo wa fahamu. Hata...

64
0