Ticker

6/recent/ticker-posts

Madhara baada ya kutumia p2,Fahamu hapa



Madhara baada ya kutumia p2,Fahamu hapa

Fahamu P2 ni dawa ya dharura yaani kwa kitaalam hujulikana kama emergency contraceptive pill, dawa hii inazuia mtu asipate Mimba kwenye mazingira ambayo umefanya mapenzi pasipo kupanga na upo siku za hatari,au umelazimishwa kufanya mapenzi au umebakwa,ili kuzuia mimba zisizotarajiwa unalazima Kunywa hizi dawa.

Ukweli ni kwamba dose ya hormones ndani ya p2 ni kubwa kuliko vidonge vya kawaida vya Uzazi(birth control pills) kitu ambacho kinaifanya isifae kwa Matumizi ya kila siku,

Hii husababisha madhara Zaidi kwa Mtu mwenye mazoea ya kuzitumia mara kwa mara. Na moja ya madhara ni mzunguko wako wa hedhi kuathiriwa sana – Periods yako inaweza isitoke kama kawaida, inaweza kuwa nyingi,zito sana,isiyoeleweka(Irregular bleeding) n.k.

Pia baadhi ya Wanawake huongezeka uzito, Hivo basi P2 haishauriwi kabsa kwa matumizi ya kila siku au kutumia kama njia ya uzazi wa mpango ya muda mrefu.

Madhara baada ya kutumia p2,

Haya ni baadhi ya Madhara au matokeo baada ya kutumia p2(emergency contraceptive pills):

  • Kupata kichefuchefu
  • Kutapika
  • Mwili kuchoka Sana
  • Kupata kizunguzungu
  • Kupata maumivu ya kichwa
  • Kupata maunivu ya tumbo
  • Maziwa kuuma au kuvuta zaidi
  • Kubadilika kwa hedhi yako ya kawaida,ikiwemo kuvuja damu nyingi au kwa muda mrefu,au kuvuja katikati ya mzunguko n.k

Kutokwa na Vitone vya damu mara kwa mara(spotting) – Unaweza kupata vitone vya damu ndani ya wiki ijayo baada ya kumeza kidonge cha dharura cha kuzuia mimba yaani P2,

Pia, hedhi yako inayofuata inaweza kuwa nyepesi au nzito, ikawahi kutoka mapema au kuchelewa kuliko kawaida. Hakikisha unapata Msaada wa Tiba ikiwa unakutana na changamoto hizi.

Mzunguko wa hedhi usio wa kawaida(Irregular menstrual cycle) – Kwa sababu ya tembe za dharura za kuzuia mimba(p2), kipindi chako cha hedhi kinaweza kufika mapema au kuchelewa, jambo ambalo hutokea sana kwa wanawake wanaotumia vidonge hivi. Hata hivyo, unapaswa kufanya kipimo cha ujauzito ikiwa hupati kipindi chako cha hedhi ndani ya wiki mbili za tarehe inayotarajiwa.

MADHARA YA KUTUMIA P2

P2 Ni Dawa iliyotengenezwa kutumiwa mara chache tu,inapokulazimu.Sio dawa unayotakiwa kutumia kama njia ya uzazi wa mpango ya muda mrefu. Kuna wanawake humeza p2 kila mwezi,hii haitakiwi. Katika mazingira ya kawaida,haipaswi kumezwa zaidi ya mara 3 kwa mwaka. Kuendekeza kila mwezi kunywa hizi p2 sio sahihi,Unatakiwa ende hospitali ili upate njia sahihi ya uzazi wa mpango ya muda mrefu.

Baadhi ya Side effects/madhara ni ya matumizi holela ya dawa hizi ni

1.Unaweza kujisikia kichefuchefu au kutapika baada ya kumeza,

2.Maumivu ya tumbo

3.Matiti kuuma na kujaa

4.Pia hedhi zako zinazofuata zinaweza zikawahi au zikachelewa au zikatoka nyingi sana( ukiona zimezidi siku 8 fika muone daktari) au ukawa unapata hedhi nyepesi sana,au pia haupati hedhi kabisa (amenorhoea)

5.Kichwa kuuma na kizunguzungu

6.Mabadiliko ya Ute ukeni (change in cervical secretion,hapa unakuta Ute wa ovulation mtu hapati).

7.Kupata maambukizi ukeni,vaginal infections

8.Hatari ya kupata PID

9.Maumivu wakati wa sex(dyspareunia)

10.Mama anakuwa hatarini kutungisha mimba nje ya kizazi yaani ectopic pregnancy.

11.Lakini pia kuna wanawake hupata Ovarian cyst,vivimbe kwenye mfuko wa mayai.

Kuna sababu hapo juu kama PID,kutopata UTE,infections kwenye uke hizi zinakuja athiri mwanamke anakuwa anapata taabu kwenye Kupata mimba

Kama hujapanga kupata mimba,tafadhari fuata njia ya uzazi wa mpango ya muda mrefu inayokufaa,achana na kumeza p2 kila mwezi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments