Connect with us

Uzazi/Ujauzito

Jinsi ya kudhibiti hali ya kuvimba miguu kwa mama mjamzito

Avatar photo

Published

on

Jinsi ya kudhibiti hali ya kuvimba miguu kwa mama mjamzito.

Swala la kuvimba miguu kwa mama mjamzito ni kawaida, na hii hutokana na kiwango Zaidi cha maji kujikusanya sehemu za chini ya mwili kama vile kwenye miguu,

Hali hii hutokea hasa ukiwa kwenye hali ya Joto, Umesimama kwa muda mrefu au kukaa kwa muda mrefu.

Pia mgandamizo au pressure ya kiumbe kinachokuwa tumboni huweza kuathiri mtiririko wa damu kwenye miguu yako. Hali hii inaweza kupelekea maji Zaidi kujikusanya kwenye miguu na kusababisha tatizo la miguu kuvimba.

Kuvimba kwa miguu (edema) ni jambo la kawaida kwa wanawake wajawazito, hasa katika trimester ya mwisho.

ANGALIZO; kuvimba miguu sana sio hali ya kawaida,hii inaweza kuwa kiashiria mojawapo cha matatizo ya Ujauzito kama vile; Kifafa cha Mimba

Hata hivyo, kuna njia kadhaa ambazo mama mjamzito anaweza kutumia kudhibiti hali hii ya kuvimba Miguu:

Jinsi ya kudhibiti hali ya kuvimba miguu kwa mama mjamzito.

– Punguza muda wa kusimama:

Jaribu kupunguza muda unaotumia kusimama mfululizo. Kama kazi yako inahitaji usimame sana,

jaribu kutafuta muda wa kukaa chini au kutembea kidogo kusaidia kusukuma damu iliyoko kwenye miguu kurudi juu.

– Pumzika na miguu iwe juu:

Unapopata nafasi ya kupumzika, lala chali na weka miguu yako juu kwa kutumia mto. Hii inasaidia kurudisha damu kwenye mzunguko na kupunguza uvimbe.

– Fanya Mazoezi ya Mwili:

Mazoezi mepesi, kama vile kutembea, kuogelea, au yoga wakati wa Ujauzito, yanaweza kusaidia kuboresha mzunguko wa damu na kupunguza uvimbe.

– Vaa viatu visivyokubana Sana:

Viatu vinavyokubana sana vinaweza kuzuia mzunguko wa damu na kusababisha miguu kuvimba zaidi.

Vaa viatu ambavyo havikubani ili kutoa nafasi ya miguu kupanuka.

Epuka kabsa kuvaa viatu virefu maarufu kama “high heels”.

– Epuka kuvaa nguo zinazobana sana:

Nguo zinazobana sana, hasa kwenye kiuno na miguu, zinaweza kuzuia mzunguko wa damu na kuchangia katika uvimbe wa Miguu.

– Kula chakula chenye afya:

Kula chakula chenye afya, kikiwa na virutubisho kama vile potassium nyingi,mfano kama vile ndizi, na kupunguza ulaji wa chumvi kunaweza kusaidia kudhibiti uvimbe wa miguu.

– Kunywa maji mengi:

Kunywa maji ya kutosha kunaweza kusaidia kutoa sodiamu na toxini nyingine mwilini ambazo zinaweza kuchangia uvimbe wa miguu.

– Usikunje miguu unapokaa:

Kukunja miguu ukiwa umekaa,maarufu kama kukunja NNE,kunaweza kuzuia mzunguko wa damu na kusababisha miguu kuvimba.

– Massage:

Massage ya miguu na miguu inaweza kusaidia kuboresha mzunguko wa damu na kupunguza uvimbe wa miguu.

NB: Ikiwa uvimbe unazidi zaidi kwa ghafla, au unahusishwa na dalili nyingine kama maumivu makali, kuchanganyikiwa, au matatizo ya kuona, ni muhimu sana kuwasiliana na daktari wako mara moja kwani hii inaweza kuwa ishara ya preeclampsia, hali ya hatari inayohitaji uangalizi wa daktari.

AU KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU NA TIBA TUWASILIANE KUPITIA NAMBA +255758286584.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...