Connect with us

Elimu&Ushauri

Sifa za Baba Bora ni Zipi?, Fahamu hapa kwa kina

Avatar photo

Published

on

Sifa za Baba Bora ni Zipi?, Fahamu hapa kwa kina

Utafiti uliochapishwa katika tovuti ya Psychology Today unaonyesha kuwa watoto ambao wapo karibu na baba zao wana hali ya kujiamini na wanaona wako salama na kadiri wanavyozidi kuwa wakubwa uhusiano wao na wazazi unazidi kuimarika.

Pamoja na umuhimu huo wakati mwingine wababa hawasimami kwenye nafasi zao hali inayofanya taratibu thamani yao kupungua na hata kutoweka kabisa na kuacha thamani hiyo itawale upande mmoja.

Mwanasaikolojia Christian Bwaya anasema katika siku za mwanzo za maisha ya mwanadamu, nafasi ya mama katika makuzi haina mjadala.

Anasema mtoto anahitaji vingi kutoka kwa mama kuanzia mahitaji ya kimwili, mahusiano, hakikisho la usalama na kadhalika, kwa msingi huo hata tabia nyingi za ukubwani zinategemea na kiwango cha ukaribu na mama.

“Kwa lugha rahisi mama ndiye anayejenga msingi wa namna tutakavyokuwa baadae kitabia. Hii ndio sababu kwa wengi wetu, mama ndiye alama ya utu wetu.

“Hata tunapojikwaa tunaita mama. Ukiangalia hata wanaume wengi, kama alikuwa na mahusiano mazuri na mama, hutafuta mke anayebeba taswira ya mama yake,”anasema Bwaya.

Hata hivyo mwanasaikolojia huyo anafafanua kuwa hali hiyo haimaanishi kuwa mtoto hamhitaji baba yake.

Anasema mwanamke anapokuwa na mahusiano yenye sonona na magomvi hawezi kuwa na furaha na hilo litaonekana ukitazama tabia ya mwanae.

“Kwa maneno mengine, kama baba anataka kuwa na ushawishi kwa mwanae, kazi kubwa ya kwanza ya kufanya ni kuhakikisha kuwa mke wake ana furaha.

“Uso wa mama wenye furaha unamjenga mtoto kuwa mtu anayejiamini. Lakini pia, mtoto anapopata ufahamu, kazi kubwa ya baba ni kumjenga mwanae kiakili.”

Baba anapaswa kufanya nini

Bwaya anasema uwezo wa mtoto kutambua mema na mabaya na kujenga msimamo wa maisha unamtegemea yeye hivyo inahitajika sauti yake kuyaingiza hayo kwenye moyo wa mtoto.

Ili sauti hii ya baba isikike vizuri na mtoto aamini kile anachoelekezwa na baba yake, ni muhimu itanguliwe na upendo na anapaswa kutambua kuwa ana nafasi ya kumjenga mtoto ikiwa atakuwa karibu na mtoto tangu mapema.

“Ukaribu una maana ya kupatikana, kuwa na mazungumzo na mtoto, kumsikiliza hisia zake na kumwelekeza pale inapobidi. Pia, baba ana kazi kubwa ya kujenga uhakikisho kwa mtoto.

“Hapa tuna maana ya baba kumhakikishia mtoto ile thamani kama binadamu, kumfanya mtoto ajione ni mtu wa maana, anayejitosheleza kama binadamu kamili. Baba akilifanya hili vizuri, mtoot hujenga hali ya kujiamini na ujasiri na matokeo yake ni kuwa karibu zaidi na baba.”anasema Bwaya.

Mwanasaikolojia huyu anaeleza kuwa baba anayemkemea mtoto mara kwa mara, anayefoka na kunyong’onyeza mtoto anamfanya mtoto ajione hana thamani na matokeo yake hujiweka mbali naye.

“Kwa msingi huo, pamoja na kukemea na kuonya pale inapobidi, ni muhimu baba kuwa mtu wa kupongeza, kuona jema kwa mtoto na kulisema. Hili likifanyika vizuri, mtoto huona thamani ya baba yake”anasema.

Mchungaji na mshauri wa masuala ya familia Richard Hananja anasema baba bora ni yule anayebeba wajibu wa familia yake na kuitunza kama ambavyo vitabu vya dini vimekuwa vikieleza.

“Baba anatakiwa kujitoa kwa moyo wake kuitunza familia yake hili anapaswa kufanywa bila kulazimishwa tofauti na ilivyo sasa ambapo wengi wamekuwa wakifanya hivyo kwa kulazimishwa. Inashangaza siku hizi unakuta baba anajiondoa kwenye jukumu la kutunza familia yake kisa mama anafanya kazi, hii si sawa baba unapaswa kuonyesha nafasi yako ili hata watoto wajifunze kutoka kwako,”

Sifa nyingine ya baba kulingana na mchungaji huyo ni kutoa majibu ya maswali yanayoikumba familia, kwa kufanya hivyo anajijengea heshima na thamani si tu kwa watoto bali hata mke.

“Sasa usitengeneze mazingira kwamba kila wanachotaka watoto wanakimbilia kwa mama yao na wanakipata ila wewe kila siku huna, hapa utaitengeneza dharau ndiyo tunasikia wanaume wanalalamika kwamba wanawake wanawadharau,”.

Anasema ni muhimu kwa baba kupata muda wa kutosha wa kuwa na watoto ili awajenge katika mfumo unaofaa kinyume na hapo atakutana na watu wengine nje watakaowapandikiza yasiyofaa.

Mchungaji Hananja anaeleza, “ Sauti ya baba ni muhimu kwenye familia, wewe kama baba una nafasi ya kumjenga mtoto wako vile unataka, mtengenezee mwelekeo wa maisha. Mtoto kuanzia mwaka 0 hadi 7 ndiyo umri wa kumtengeneza sasa kama huna muda wa kukaa naye ukapandikuza vitu vizuri ndani yake tegemea watu wengine kufanya hivyo,”.

Mawazo mchanganyiko

Deus Ngoba mkazi wa Madale anasema wababa wengi hawana muda wa kukaa na watoto wakiamini jukumu hilo ni la mama na wao kazi yao ni kuwatafutia mahitaji jambo linalowafanya wawe mbali na familia.

“Usiogope kutumia muda wako vizuri na mwanao wa kike au wa kiume na kucheza nao na kuwabembeleza wanapolia. Watoto siku zote hukumbuka matendo haya na hivyo kujenga upendo kati yenu na kuzidisha amani kwa familia. Ni vyema kuhamasishana wake kwa waume ili kila mmoja wetu ajione ana uwezo wa kutekeleza majukumu ya malezi.

“Kingine jenga heshima na upendo kwa watoto wako na siyo nguvu. Kila mtu hufurahia kupenda na kupendwa na unaweza kupata upendo wa watoto wako kwa kuwapenda na si kwa kuwaonesha mabavu. Ukiwa mbambe utaishia kupata nidhamu ya uoga na sio heshima na utii wa kweli. Ukiwa kama baba onyesha upendo, heshima na uwajibikaji kwa watoto, mwenza wako na familia kwa ujumla. Kumbuka kwa kufanya hivi unajenga msingi wa tabia za mwanao unayemtaka,”

Kwa upande wake Suzan Mhilu mkazi wa Buza anasema baba bora anapaswa kuishi kwa mfano ili watoto wake waige na kujifunza vitu kutoka kwake.

Anasema kama baba atakuwa anaonyesha vitendo vizuri mbele ya mtoto itamfanya aishi katika mfumo huo na hilo itasaidia watoto kujua umuhimu wa kufikia maamuzi kwa mazungumzo kwa maana ya kutambua kuwa kuna kukubaliana na kutokukubaliana.

Usuli

Siku hii ilianza kuadhimishwa Spokane, Washington nchini Marekani mwaka 1910 na Sonora Smart Dodd mzaliwa wa Arkansas. Baba yake William Jackson Smart alikuwa mwanajeshi wa zamani na aliwalea watoto sita akiwa kama mzazi pekee.

Baada ya miaka kadhaa tangu kuadhimishwa kwa siku hii huko Marekani hatimaye ujumbe ukafika dunia nzima na mataifa mbalimbali yakaanza kuadhimisha siku hii kwa lengo la kuwaenzi kina baba wanaojitoa kwa hali na mali katika malezi ya watoto.

Via:Mwananchi.

Karibu AfyaUpdates Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In https://afyaclass.com  Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa4 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa8 hours ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa4 days ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa3 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa3 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa4 weeks ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa4 weeks ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Magonjwa1 month ago

Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga

“Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga” Kifo cha ghafla ni janga lisilotarajiwa ambalo linaweza kumpata...

Trending