Connect with us

Events

Angalizo utoaji wa Dawa za Semaglutides,baada ya dawa bandia kuongezeka

Avatar photo

Published

on

Hii ni notisi ya kwanza rasmi iliyotolewa na WHO baada ya kuthibitisha baadhi ya ripoti hizo.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari WHO imeeleza kuwa tahadhari hiyo ni kwa ajili ya makundi matatu ya bidhaa ya Semiglutide hususan kwa chapa ya Ozempic ambayo wameeleza imegundulika huko nchini Brazili mwezi Oktoba 2023, Uingereza na Ireland Kaskazini mwezi Oktoba 2023, na Marekani mwezi Desemba 2023.

Mfumo wa Ufuatiliaji na Uangalizi wa WHO (GSMS) umekuwa ukiangalia ongezeko la ripoti kuhusu bidhaa zisizo halisi (feki) za semaglutide katika maeneo yote ya kijiografia tangu mwaka 2022.

Mkurugenzi Mkuu Msaidizi wa WHO wa Upatikanaji wa Dawa na Bidhaa za Afya Dkt. Yukiko Nakatani

Amewashauri wataalamu wa afya na mamlaka za udhibiti na umma kufahamu kuhusu makundi haya ya dawa zisizo halisi, “Tunatoa wito kwa wadau kuacha matumizi yoyote ya dawa zinazotiliwa shaka na kutoa taarifa kwa mamlaka husika”.

Uhaba wa dawa wachangia bidhaa bandia

Dawa hizi za Semaglutides, pamoja na bidhaa maalum za chapa ambayo si halisi zinatolewa kwa wagonjwa wa kisukari cha aina ya 2 ili kupunguza viwango vyao vya sukari kwenye damu. Semaglutides pia hupunguza hatari ya magonjwa ya moyo na mishipa.

Bidhaa nyingi za semaglutide zinapaswa kudungwa chini ya ngozi kila wiki lakini pia zinapatikana kama vidonge vya kumeza kila siku.

Katika nchi nyingine dawa hizi zimeonesha kupunguza hamu ya kula pamoja na kupunguza viwango vya sukari ya damu, na kwa hivyo zinazidi kuagizwa kwa ajili ya matumizi ya kusaidia kupunguza uzito wa mwili kwa watu.

WHO imekuwa ikifuatilia kwa ukaribu ongezeko la mahitaji ya dawa hizi pamoja na ripoti kuhusu bidhaa bandia. Bidhaa hizi zisizo halisi zinaweza kuwa na madhara kwa afya ya watu; dawa bandia zinaweza kusababisha matatizo makubwa ya kiafya.

Katika hali nyingine, kiungo tendaji ambacho hakijatangazwa kinaweza kuwa kwenye kifaa cha sindano, kama insulini, na kusababisha anuwai isiyotabirika ya hatari za kiafya au shida.

Semaglutides si sehemu ya matibabu yanayopendekezwa na WHO kwa ajili ya udhibiti wa kisukari kutokana na gharama yake kuwa ya juu kwa sasa. Kizuizi cha gharama kinafanya bidhaa hizi kutofaa kama mbinu ya afya ya umma.

Pia, kuna matibabu ya bei nafuu zaidi yanayopatikana kwa ugonjwa wa kisukari, na yana matokeo sawa na yale ya semaglutides kwenye sukari ya damu na hatari ya moyo na mishipa.

Wito kwa watu wote

Ili kujilinda dhidi ya dawa zisizo halisi na madhara yake, wagonjwa wanaotumia bidhaa hizi wanaweza kuchukua hatua kama vile kununua dawa kutoka kwa madaktari walio na leseni na kuepuka kununua dawa kutoka kwa vyanzo visivyojulikana au ambavyo havijathibitishwa.

Watu wanapaswa kuangalia vifungashio na tarehe za mwisho wa matumizi ya dawa wanapozinunua, na watumie bidhaa kama ilivyoelekezwa.

Watumiaji wa semaglutides ya sindano, wanapaswa kuhakikisha kuwa wamehifadhiwa kwenye jokofu.

Iwapo utagundua dawa uliyonunua ni bandia unaweza kuwajulisha WHO kupitia barua pepe rapidalert@who.int.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa4 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa7 hours ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa4 days ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa3 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa3 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa4 weeks ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa4 weeks ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Magonjwa1 month ago

Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga

“Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga” Kifo cha ghafla ni janga lisilotarajiwa ambalo linaweza kumpata...

Trending