Ticker

6/recent/ticker-posts

Dalili za ukimwi kwenye ngozi,zifahamu hapa



Dalili za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala hii ili kujua mabadiliko mbali mbali ambayo hutokea kwenye ngozi baada ya mtu kupata maambukizi ya virusi vya Ukimwi(VVU).

Takriban asilimia 90% ya watu wanaoishi na virusi vya HIV hupata mabadiliko kwenye ngozi na dalili kwenye hatua fulani wakati wa ugonjwa wao.

Ingawa,kukiwa na udhibiti mzuri wa virusi na uimarishaji wa mfumo wa kinga ya mwili matatizo haya ya ngozi hayatokei kwa kiwango kikubwa. Pia hata yakitokea hayaleti madhara makubwa na ni rahisi kuyatibu.

Dalili za ukimwi kwenye ngozi

Moja ya dalili kubwa kwenye ngozi za Maambukizi ya Virusi vya Ukimwi ni pamoja na;

1. Mtu kuwa na vipele au Rashes kwenye ngozi

Upele kwenye ngozi ni mojawapo ya dalili ya kawaida kwa mtu mwenye maambukizi ya VVU, kama dalili kubwa inayohusiana na ngozi.

Mara nyingine, ngozi inaweza kuathiriwa na vitu vingi kama vile,kemikali,allergies,Fangasi na mwanga wa jua pia, lakini Wakati mwingine vipele husababishwa na VVU.

Upele wa kawaida kwa maambukizi ya VVU mara nyingi hutokea eneo tambarare kwenye ngozi ambalo limefunikwa na matuta madogo,

Pia Mzio au allergic reactions kwenye ngozi huweza kuonekana katika muda wa wiki moja hadi mbili baada ya kuanza dawa mpya.

Upele huu kwenye ngozi pia unaweza kutokana na sababu zingine ikiwemo;

  • Tatizo la Molluscum contagiosum,
  • Maambukizi ya herpes simplex
  • herpes zoster infections,
  • Madhara ya dawa(drug eruptions),
  • Au Kaposi sarcoma lesions.
  • Pia upele kwenye ngozi kwa mtu mwenye HIV unaweza kuwa matokeo ya dawa anazotumia ili kupambana na HIV.

2. Kuwa na malengelenge kwenye ngozi au mkanda wa jeshi(Shingles)

Pia mtu mwenye maambukizi ya Virusi vya Ukimwi(VVU) anaweza kupata vipele vipele vinavyokuwa kama malengelenge kwenye ngozi ambavyo pia husababisha maumivu makali, aina hii ya vipele(painful, blistering skin rash) hujulikana kama,”Shingles”,

Na kwa Sababu vinakuwa vya kufuatana eneo moja la mwili au upande mmoja wa mwili vikapatiwa jina kama “mkanda wa Jeshi”. Soma Zaidi hapa

Shingles chanzo chake ni maambukizi ya virusi vya herpes zoster virus.

Pia mabadiliko kwenye ngozi huweza kutokana na muitikio wa kinga ya mwili dhidi ya kuamshwa upya kwa virusi aina Chickenpox virus, ambavyo vilikuwa dormant mwilini toka utotoni.

Mara nyingi mkanda wa Jeshi(Shingles) hutokea maeneo kama vile;

  • Kifuani
  • Maeneo ya tumboni
  • Kwenye ubavu
  • Mgongoni
  • Na hata kwenye eneo la nyonga,Pelvis

Ni mara chache sana mkanda wa jeshi kutokea maeneo kama vile; miguuni, mikononi, au usoni.

Mkanda wa Jeshi; ni miongoni mwa dalili za kwanza kwenye Ngozi ambazo huashiria mtu kuwa na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi(VVU),

Ingawa watu wengi hawafahamu kuwa,Mkanda wa jeshi ni kiashiria pia kwamba kinga yako ya mwili ni dhaifu.

Hii ina maana,Sio kila mwenye mkanda wa Jeshi basi ana maambukizi ya Virusi vya Ukimwi, Zipo sababu zingine za kutokea kwa mkanda wa jeshi. Soma Zaidi hapa chanzo cha Mkanda wa Jeshi;

3. Tatizo la Lesions kwenye ngozi

Tazama picha hizi, huu ndyo mfano wa Lesions kwenye ngozi;

Na chanzo chake ni maambukizi ya Virusi ikiwemo HIV(viral infections).

Maambukizi ya virusi kama vile Herpes simplex I na II ni chanzo kikubwa cha tatizo hili la lesions kwenye ngozi, na hutokea eneo lolote la ngozi. Hali hii huweza kupona ndani ya wiki moja mpaka mbili.

kumbuka; Matokeo ya ngozi kuathiriwa ikiwa mtu ana maambukizi ya Virusi vya Ukimwi ni kwa sababu ya kinga ya mwili kuwa dhaifu,

Hii husababisha maambukizi mengine mbali mbali kama vile; Kaposi sarcoma, thrush, pamoja na herpes, ambapo husababishwa na vimelea vingine kuchukulia faida udhaifu huu wa kinga yako ya mwili.






Post a Comment

0 Comments