Ticker

6/recent/ticker-posts

Mwanaume achanjwa mara 217 dhidi ya Uviko ndani ya miezi 29



Mwanaume achanjwa mara 217 dhidi ya Uviko ndani ya miezi 29.

Mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 62 kutoka Magdeburg, Ujerumani, “kwa makusudi na kwa sababu za kibinafsi“ alichanjwa mara 217 dhidi ya Uviko ndani ya miezi 29.

Ushahidi ulikusanywa na mwendesha mashitaka wa Magdeburg, aliyeanzisha uchunguzi wa madai ya ulaghai lakini hakufungua mashitaka ya jinai.

Watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Erlangen-Nuremberg wamemfanyia vipimo mbalimbali mwanamume huyo kuchunguza madhara ya kinga ya mwili.

Mwanamume huyo “hakuripoti madhara yoyote yanayohusiana na chanjo,” waliandika katika jarida la sanyansi la Lancet.

Hakukuwa na dalili kwamba amewahi kuambukizwa Covid, hata hivyo.

>>Soma Zaidi kuhusu; Ugonjwa wa COVID-19



Post a Comment

0 Comments