Ticker

6/recent/ticker-posts

Polisi waokoa watoto 251 katika dhehebu tata nchini Zimbabwe



Polisi waokoa watoto 251 katika dhehebu tata nchini Zimbabwe.

Watoto waliookolewa “walikuwa wakitumiwa kufanya shughuli mbalimbali kwa manufaa ya kiongozi wa dhehebu”, taarifa ya polisi ilisema.

Polisi walisema wengi wa watoto hao 251 waliopatikana katika shamba la Ishmael Chokurongerwa, 56 huko Nyabira, hawakuwa na vyeti vya kuzaliwa na hawakuruhusiwa kuhudhuria shule.

Polisi pia waligundua kaburi katika shamba hilo ambapo watu 16 wamezikwa kwa siri, wakiwemo watoto wachanga saba.

Mmoja wa washiriki wa madhehebu hayo aliwaambia waandishi kwamba elimu rasmi shuleni haitakiwi na Mungu “kwa sababu ni kinyume na mafundisho ya Mungu”.



Post a Comment

0 Comments