Ticker

6/recent/ticker-posts

Wafanyakazi kulipwa dola 75,000 kwa kila mtoto atakayezaliwa



Wafanyakazi kulipwa dola 75,000 kwa kila mtoto atakayezaliwa.

Kampuni moja ya Korea Kusini imeahidi kulipa wafanyakazi hadi kiasi cha $75,000 kwa kila mtoto atakayezaliwa, ikiwa ni juhudi za kusaidia kuinua kiwango cha watoto wanaozaliwa nchini humo.

Serikali ya Korea Kusini na makampuni mengine binafsi yamekuwa yakitoa marupurupu ya kifedha ili kuhimiza watu kupata watoto zaidi, lakini hakuna kampuni inayotoa kiwango kikubwa kama Booyoung Group.

Booyoung Group, kampuni ya ujenzi iliyoko Seoul ilisema wanufaika ni pamoja na wanaume na wanawake.

Je vipi kama utaratibu huu ukija nchini kwako, utapanga kupata watoto wangapi?



Post a Comment

0 Comments