Ticker

6/recent/ticker-posts

Clarithromycin inatibu nini, soma hapa kufahamu



Clarithromycin inatibu nini

Clarithromycin ni dawa inayotumika kutibu aina nyingi za maambukizi yanayotokana na bacteria(bacterial infections).

Dawa hii pia huweza kutumika pamoja na dawa zingine za vidonda vya tumbo(anti-ulcer medications) kutibu aina kadhaa za vidonda vya tumbo.

Clarithromycin huweza kuzuia aina nyingi za maambukizi ya bacteria, na dawa hii hujulikana kama macrolide antibiotic. Hufanya kazi kwa kuzuia ukuaji wa bacteria.

Kumbuka; Clarithromycin haitafanya kazi dhidi ya maambukizi yoyote yanayotokana na virusi-viral infections.

Dawa ya Clarithromycin huweza kutumika kutibu maambukizi ya kifua kama vile ya; pneumonia, matatizo ya ngozi kama vile cellulitis, pamoja na maambukizi ya Sikio. Pia  Clarithromycin huweza kutumika kutibu Helicobacter pylori, bacteria anayesababisha vidonda vya Tumbo.

Wakati mwingine Clarithromycin hutumika kwa watu wenye mzio au allergy na dawa jamii ya penicillin au antibiotics zinazofanana na penicillin, kama vile amoxicillin.

Unaweza kupewa Clarithromycin kwa maambukizi ya bacteria kwenye mapafu mfano kwa mgonjwa wa pneumonia, maambukizi kwenye mrija unaolekea kwenye mapafu-bronchitis (infection of the tubes leading to the lungs), maambukizi ya masikio,Ngozi,Koo n.k

Dawa hii ya Clarithromycin huweza kutumika kutibu na kuzuia kusambaza kwa maambukizi ya Mycobacterium avium complex (MAC) [aina ya maambukizi ya mapafu ambayo mara nyingi huathiri watu walio na virusi vya ukimwi (VVU)].

DOSES;

Kwa Upande wa Doses, Lazima ushauriane na wataalam wa afya,kwani itategemea na umri wako,Uzito, tatizo linalokusumbua, hali yako ya kiafya pamoja na uwezo wa mwili wako kujibu matibabu.

Ikiwa unatumia dawa hii kutibu maambukizi, endelea kutumia dawa hii hadi kiasi kamili kilichowekwa kiwe kimekamilika, hata kama dalili zitatoweka baada ya siku chache. Kuacha dawa mapema kunaweza kusababisha kurudi kwa maambukizi. Mwambie daktari wako ikiwa hali yako hudumu au inazidi kuwa mbaya.

Maudhi(Side Effects) ya Clarithromycin

Haya hapa ni maudhi yanayoweza kutokea kwa Mtu anayetumia dawa ya Clarithromycin;

  1. Kuharisha
  2. Kuhisi kichefuchefu
  3. Kutapika
  4. Kupata maumivu ya kichwa
  5. Kubadilika kwa ladha mdomoni n.k

Watu wengi wanaotumia dawa hii hata wakipata baadhi ya Side effects hizi, hawapati kwa kiwango kibaya.

Hakikisha unaongea na wataalam wa afya ili kuacha na kubadilishiwa mara moja dawa hii ya Clarithromycin ikiwa baada ya kutumia;

– Unapata kichefuchefu na kutapika bila kukoma

– Unapoteza uwezo wako wa Kusikia

– Unapata dalili zote za kuchanganyikiwa au matatizo ya akili

– Unapoteza uwezo wa kuona vizuri, unaona marue rue n.k

– Misuli inakuwa Dhaifu

– Unapoteza uwezo wa Kuongea

– Unapata maumivu makali sana ya Tumbo

– Unakojoa Mkojo mweusi

– Ngozi na macho vinabadilika rangi na kuwa manjano.

– Unapata homa ambayo haiishi

– Unavimba lymph node,

– Unaaza kutokwa na vipele kwenye ngozi

– Unakosa pumzi au kupata shida ya kupumua

– Unapata kizunguzungu

– Unaaza kupata muwasho mkali kwenye ngozi,usoni,kwenye Ulimi,kooni n.k.

Rejea Link;



Post a Comment

0 Comments