Ticker

6/recent/ticker-posts

UTAFITI: Waishio kando ya Bahari wana afya bora



UTAFITI: Waishio kando ya Bahari wana afya bora

Kwa mujibu wa utafiti uliyofanywa na Dk Lewis Elliott kutoka Chuo Kikuu cha Exeter nchini Uingereza umebaini kuwa watu wanaoishi karibu na mazingira ya ufukwe (kando ya bahari) wana afya bora kuliko waishio mbali na fukwe.

Utafiti huo ulibaini kuwa waishio kando ya bahari wako na hali nzuri ya mwili na akili utafiti huo ukijumuisha watu wanaoishi chini ya kilomita moja hadi wale walio zaidi ya kilomita 50.

Aidha utafiti huo ulimaliza kwa kueleza kuwa kuishi karibu na bahari kunamarisha afya yako kutokana na kuwepo na upepo asili na mazingira tulivu hivyo basi yanayokufanya ujiskie vizuri.



Post a Comment

0 Comments