Ticker

6/recent/ticker-posts

Madhara ya kufanya Mapenzi wakati wa PERIOD au HEDHI,kwa mwanaume na mwanamke



Madhara ya kufanya Mapenzi wakati wa PERIOD au HEDHI

KUNA MADHARA YA KUFANYA TENDO LA NDOA WAKATI WA PERIOD

Watu wengi hawajui kwamba hata kama ni mke wako umemuoa ndani,sio salama kufanya naye mapenzi akiwa siku za hedhi au period, Kuna madhara mengi kiafya kwa mwanaume na kwa mwanamke pia endapo watashiriki tendo la ndoa wakati wa hedhi.

MADHARA YA KUFANYA TENDO LA NDOA WAKATI WA PERIOD AU HEDHI KWA MWANAUME.

– Kuwa katika hatari ya kupatwa na shida ya kuziba mrija wa Mkojo

– Kuwa katika hatari yakupata magonjwa hasa hasa katika njia ya mkojo kwani period ni uchafu unaotoka ndani ya mwanamke huku ukiwa na vitu mbali mbali hata vimelea vya magonjwa vikitolewa nje ya mwili.

– Pia Tezi dume huweza kuathirika kutokana na mwanaume kufanya mapenzi mwanamke akiwa siku za period

– Kutokufurahia tendo la ndoa kutokana na kulifanya katika mazingira machafu ya damu,harufu N.k

– Hatari ya kutokumridhisha unayefanya nae tendo la Ndoa

MADHARA YA KUFANYA TENDO LA NDOA WAKATI WA PERIOD AU HEDHI KWA MWANAMKE.

• Kama unashida ya kuumwa na tumbo wakati wa hedhi,ukifanya mapenzi wakati ukiwa kwenye hedhi,badala ya kufurahia tendo la ndoa,utapata maumivu makali kupita kawaida

• Kuwa katika hatari ya kupata magonjwa kama vile maambukizi katika via vya uzazi au kwa kitaalam Pelvic Inflammatory disease(PID), kwani uchafu ambao umechanganyika na vimelea vya magonjwa badala ya kutolewa nje,utarudishwa ndani na kuanza kuleta athari katika maeneo mbali mbali kama vile; shingo ya kizazi N.K

• Kufanya mapenzi wakati wa hedhi huweza kuongeza uwezekano wa mwanamke kublid kupita kawaida.

• Mwanamke kupata Maumivu makali ukeni akishiriki tendo la ndoa wakati wa hedhi kutokana na uvimbe wa kuta au mashavu ya uke Wakati wa hedhi

• Kuwa katika hatari ya kutoridhika au kutokufurahia tendo la Ndoa kabsa.

EPUKA TABIA HII YA KUFANYA MAPENZI WAKATI WA HEDHI Kwani ni hatari kwa Afya Yako…!!!!

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments