Ticker

6/recent/ticker-posts

Je Mtoto Hurithi Akili Kutoka Kwa Mzazi Yupi?



JE MTOTO HURITHI AKILI KUTOKA KWA MZAZI YUPI?

Utafiti katika panya uligundua seli ambazo zilikuwa na genes za mama au za baba pekee katika sehemu sita tofauti kwenye ubongo. 

Sehemu hizo zilidhibiti kazi tofauti za utambuzi mfano tabia ya kula hadi kumbukumbu. .

Utafiti uliofanywa ulibainisha, seli zilizo na genes za baba zilizokusanywa katika sehemu za mfumo wa limbic, ambao unahusika katika kazi kama vile mapenzi, chakula na hasira.

Hakukua na seli za baba kwenye cortex ya ubongo, ambapo ndipo kazi za utambuzi wa hali ya juu hufanyika.

Kiwango kikubwa cha fatty acid kinachopatikana kwa wanawake kinauhusiano na uwezo wa akili wa mtoto. Wanawake wenye maumbo makubwa wanaweza kupata watoto wenye uwezo mkubwa wa kiakili. 

Kiwango cha omega 3 fatty acid na hecoxadexanoic acid husaidia ukuaji wa ubongo wa mtoto. .

Utafiti mwingine ulisema iwapo mtoto by chance akapata urithi wa kijenetiki kutoka kwa wazazi wote ( X-linked traits from both parents) basi anakuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kiakili hii hutokea kama X-linked genes kutoka kwa baba zisipozidiwa uwezo na zile za mama (masked traits) .

Utafiti mwingine ulibainisha kwamba asilimia 40-60% ya akili ya mtoto haihusiani na jenetiki/kurithi. Akili inajengwa na vitu kama mazingira, uwezo wa akili wa mama kulea na ukaribu wa mama na mtoto. .

Hili liliangaliwa kwa utafiti wa sehemu ya ubongo inayoitwa Hippocampus. Hippocampus ina kazi ya kujifunza, kumbukumbu na kukabiliana na msongo wa mawazo na hatari katika ubongo.

Watoto waliokua na ukaribu na mama zao na ambao walilelewa kwa upendo eneo hili la ubongo lilikua kubwa zaidi ukilinganisha na watoto waliokosa ukaribu na mama zao. (Credit: Dr. P.Binxete)

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



Post a Comment

0 Comments