Ticker

6/recent/ticker-posts

Ugonjwa wa Amoeba: Sababu, Dalili na Matibabu



Ugonjwa wa Amoeba: Sababu, Dalili na Matibabu

Ugonjwa wa amoeba ni ugonjwa hatari unaosababishwa na kimelea(parasite) kinachoitwa Entamoeba histolytica.

Entamoeba histolytica  ni kimelea kwenye kundi la anaerobic parasite na kwa mara ya kwanza hupatikana kwenye Utumbo mpana(colon);

Ingawa kutokana na Sababu zisizofahamika, kimelea hiki kina uwezo wa kutoka na kupita moja kwa moja mpaka kwenye Ini na kusababisha tatizo ambalo hujulikana kwa kitaalam kama amoebic liver abscesses."

Kimelea hiki kinaishi kwenye Utumbo wa binadamu na kinaweza kusababisha ugonjwa wa amoeba kwa mtu yeyote anayekula au kunywa kitu kilichoambukizwa na kimelea hiki.

Katika makala hii, tutajifunza kuhusu sababu, dalili na matibabu ya ugonjwa wa amoeba.

KUMBUKA; amoebiasis-Ndyo ugonjwa wenyewe ambao chanzo chake ni kimelea au parasite anayejulikana kama Entamoeba histolytica.

NANI YUPO KWENYE HATARI YA KUPATA UGONJWA WA AMOEBA(AMOEBIASIS)?

Ingawa mtu yoyote anaweza kuugua Ugonjwa wa amoeba, Tatizo hili huwapata sana watu ambao wanaishi kwenye mazingira machafu,

Lakini Pia baadhi ya Tafiti zinaonyesha Ugonjwa wa Amoeba(amoebiasis) huwapata sana Wanaume wanaoshiriki Mapenzi na wanaume wenzao

Sababu ya Ugonjwa wa Amoeba:

Ugonjwa wa amoeba husababishwa na kimelea kinachoitwa Entamoeba histolytica,

Kimelea hiki hupatikana kwenye kinyesi cha mtu aliyeambukizwa na kinaweza kuambukiza mtu mwingine kupitia chakula au maji yaliyoambukizwa.

Mbali na hilo, mtu anaweza kuambukizwa ugonjwa huu kwa kugusa vitu vilivyoambukizwa kwa mikono iliyochafuliwa na kimelea hiki.

Dalili za Ugonjwa wa Amoeba:

Baadhi ya dalili za ugonjwa wa amoeba ni pamoja na:

  1. Mtu Kuharisha mara kwa mara
  2. Mtu Kupata Maumivu ya tumbo
  3. Kupoteza hamu ya kula
  4. Kuhisi Kichefuchefu pamoja na Kutapika
  5. Kuhisi kizunguzungu n.k

Katika baadhi ya matukio, ugonjwa huu unaweza kusababisha matatizo makubwa zaidi ya kiafya kama vile;

  • kuvuja kwa damu kwenye utumbo
  • Pamoja na maambukizi kwenye ini.

Matibabu ya Ugonjwa wa Amoeba:

Matibabu ya ugonjwa wa amoeba hutegemea kiwango cha ugonjwa na dalili zinazojitokeza,

Dawa za kuuwa vimelea hivi vinavyosababisha Ugonjwa wa amoeba hutumiwa kutibu ugonjwa huu.

Matibabu ya maumivu ya tumbo pia yanaweza kutolewa kwa wagonjwa ambao wanapata maumivu makali.

Kwa kuongezea, lishe bora ni muhimu katika kusaidia kupona haraka kwa ugonjwa huu.

Kuzuia Ugonjwa wa Amoeba:

Kuzuia ugonjwa wa amoeba ni muhimu sana ili kuepuka madhara ya kiafya. Baadhi ya njia za kuzuia ugonjwa huu ni pamoja na:

✓ Kufuata kanuni zote za usafi wa mazingira

✓ Kunywa maji safi na salama

✓ Kula chakula kilichoandaliwa vizuri

✓ Nawa Mikono kwa Sabuni na Maji safi kabla ya kula au kunywa kitu chochote

#SOMA ZAIDI Hapa Ugonjwa wa Amiba

AMIBA

• • • • •

UGONJWA WA AMIBA(chanzo,dalili na Tiba yake)

Huu ni ugonjwa unaohusu utumbo mpana wa binadamu kushambuliwa na vimelea vya magonjwa ambavyo kwa kitaalam hujulikana kama Amoeba.

CHANZO CHA UGONJWA WA AMIBA

 Hivo basi, chanzo cha ugonjwa wa amiba ni mashambulizi ya vimelea vya amiba hasa hasa jamii ya Entamoeba histolytica.

Vimelea hivi huingia moja kwa moja kwenye mwili wa binadamu kwa kupitia mdomoni na kuenda moja kwa moja kwenye njia ya mfumo wa mmeng'enyo wa chakula mpaka kufika kwenye utumbo mkubwa.

DALILI ZA UGONJWA WA AMIBA NI PAMOJA NA;

- Mgonjwa kujisaidia kinyesi chenye vitu kama makamasi

- Mgonjwa kuanza kupata maumivu ya tumbo sana mithili ya tumbo kusokota

- Mgonjwa kuanza kujisaidia choo kilaini sana

- Mgonjwa kuharisha au kujisaidia haja kubwa ya maji maji sanaa

- Mgonjwa kujisaidia kinyesi ambacho kimechanganyika na damu

- Mgonjwa kutoa hewa kwa njia ya haja kubwa mara kwa mara(kujamba)

- Mgonjwa kupata maumivu ya tumbo,Kifua na viungo mbali mbali vya mwili

- Joto la mwili la mgonjwa kupanda au mgonjwa kuwa na Homa

- Mgonjwa kupatwa na tatizo la kupungukiwa na damu 

- Kupoteza appetite ya chakula kabsa

- Mgonjwa kupatwa na hali ya kichefu chefu pamoja na kutapika

- Mgonjwa kupungua uzito wa mwili na kukonda

KUMBUKA; Moja ya njia ya mtu kupata vimelea hivi vya amoeba ambavyo husababisha ugonjwa huu wa amiba ni pamoja na kunywa maji machafu sana.

Maji ambayo yamechanganyika ma kinyesi cha mtu ambaye alikuwa na vimelea hivi vya amoeba.

MATIBABU YA UGONJWA WA AMIBA

Zipo dawa mbali mbali ambazo hutumika kutibu ugonjwa huu wa amiba

Conclusion(Hitimisho):

Ugonjwa wa amoeba ni ugonjwa hatari unaosababishwa na kimelea kinachoitwa Entamoeba histolytica. Kimelea hiki kinaishi kwenye Utumbo wa binadamu na kinaweza kusababisha matatizo makubwa ya kiafya.

Ni muhimu kufuata kanuni zote za usafi wa mazingira na kula chakula kilichoandaliwa vizuri ili kuzuia ugonjwa huu. Kama unapata dalili za ugonjwa wa amoeba, ni muhimu kuwahi Hospital ili kupata matibabu sahihi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments