Ticker

6/recent/ticker-posts

MATATIZO YATOKANAYO NA KUSHUKA KWA KINGA YA MWILI



KINGA

• • • • • •

♣MATATIZO YATOKANAYO NA  KUSHUKA KWA KINGA YA MWILI.♣


Kwa kawaida mwili wa binadamu yeyote umeumbwa na kinga ya mwili ya asili ambayo lengo lake kuu ni kuulinda mwili dhidi ya vimelea vya magonjwa.Inapotokea kimelea (vimelea) kuingia katika mwili wa binadamu kwa njia yoyote (kunywa au kula vimelea,kugusana na majimaji au ngozi ya mtu mwenye vimelea,au kupitia damu yenye vimelea n.k), mwili hutengeneza kingamwili (antibodies) ambazo hupigana na vimelea hivyo ili kuuweka mwili katika afya njema kama hapo awali.Vile vile kwenye ngozi, mfumo wa chakula, ukeni, uumeni n.k Hata hivyo vijidudu hivi huweza kuwa chanzo cha magonjwa iwapo kinga ya mwili itashuka.

Magonjwa nyemelezi ni yale ambayo hushambulia mwili wa binadamu pale uwezo wa kinga ya mwili kupigana na vimelea vya magonjwa unaposhuka.Ni magonjwa ambayo katika hali ya kawaida hayategemewi kujitokeza kwa mtu mwenye kinga kamili ya mwili.


Magonjwa nyemelezi husababishwa na vijidudu mbalimbali kama bakteria, virusi na fangasi.Baadhi ya Magonjwa hayo ni kama yafuatayo:-

Kifua kikuu

Nimonia

Maumivu ya retina

Ugonjwa wa ngozi

Ugonjwa wa malengelenge

Mkanda wa jeshi

Homa ya UTI wa mgongo

Kuugua mara kwa mara n.k


Ni wakati wetu wote tufahamu ni jinsi gani yatupasa kuimarisha kinga zetu kwa kufuata kanuni za ulaji bora na kuachana na baadhi ya tabia ambazo zitakufanya kushuka kwa kinga ya mwili. Na kama unajua kuwa kinga ya mwili wako imeshuka basi usisite kuwasiliana nasi  ili uweze ushauri na ni vitu gani ufanye uweze kuimarisha kinga ya mwili wako.






Post a Comment

0 Comments