Ticker

6/recent/ticker-posts

MATITI YA MWANAMKE KUKOSA UWIANO



 MATITI

• • • • •

MATITI YA MWANAMKE KUKOSA UWIANO


Wakina mama wengi ambao hunyonyesha hupatwa sana na hali hii ya matiti kutofautiana ukubwa au size. Hali hii sio tatizo kwa mama anayenyonyesha kwani ni kiashiria kwamba mtoto anapenda kunyonya titi flani zaidi ya lingine.


Huna haja ya kuwa na wasi wasi ila cha msingi ni mtoto anyonye na kushiba vizuri maziwa ya mama yake. Lakini endapo hali hii unaiyona ni kero kwako, basi wakati unamnyonyesha mtoto,anza na titi dogo  na hakikisha unalitumia mara mbili zaidi ya lile kubwa.


VIPO VIASHIRIA VYA HATARI KATIKA TITI LAKO AMBAVYO NI PAMOJA NA;


1. Titi moja kuwa kubwa kuliko lingine wakati wewe hunyonyeshi


2. Chuchu ya titi lako kutoa usaha au Damu,hii sio ishara nzuri,ni mojawapo ya dalili za magonjwa kama saratani ya matiti N.K


3. Kuwa na vitu ndani ya titi ambavyo ukivishika vipo mithili ya punje ya mchele au harage


4. Kuwepo kwa ugumu ndani ya titi au maeneo ya kwapani


5. Kuwa na tatizo la michubuko pamoja na vidonda kwenye titi lako


6. Kupata maumivu ya titi yanayoendana sambamba na joto la mwili kupanda au kuwa na homa.


KUMBUKA,moja ya saratani ambazo huwasumbua wanawake wengi ni pamoja na saratani ya matiti,hivo jenga tabia ya kujichunguza mwenyewe mara kwa mara, na kugundua mabadiliko yoyote yanayoweza kutokea ndani ya titi lako kwa jumla wake.


Mbali na tatizo la Saratani ya matiti,pia titi huweza kukumbwa na tatizo la kuvimba kwa tezi ndani ya titi pamoja na titi kushambuliwa na magonjwa mengine.


Kumbuka haya kwa mama anayenyonyesha;


- Fanya usafi wa mikono yako kabla ya kumshika mtoto


- Hakikisha umeosha au kusafisha titi lako kabla ya kuanza kumnyonyesha mtoto


- Unyonyeshaji hutakiwa kwa kipindi cha miezi sita bila mtoto kuchanganyiwa maziwa ya mama na vyakula vingine


- Baada ya kipindi cha miezi sita ya maziwa ya mama pekee,anza kumchanganyia mtoto maziwa ya mama na vyakula vingine ila usiache kumnyonyesha mpaka afikishe umri wa miaka miwili au mitatu ukiweza.


NB; Maziwa ya mama ni kinga tosha kwa mtoto hasa hasa katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzoni,ambapo kinga ya mtoto dhidi ya magonjwa ipo chini sana.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.








Post a Comment

0 Comments