Ticker

6/recent/ticker-posts

MATUMIZI YA DAWA AINA YA SILDENAFIL CITRATE (VIAGRA)(kutibu uume kushindwa kusimama)



 DAWA

• • • • • •

MATUMIZI YA DAWA AINA YA SILDENAFIL CITRATE (VIAGRA)(kutibu uume kushindwa kusimama)


ni dawa inayotumika kutibu tatizo la kusimama kwa uume (erectile dysfunction) na shinikizo la damu kwenye mishipa.


  Erectile dsyfunction ni tatizo la uume kushindwa kusimama vizuri wakati wa kujamiiana au kushindwa kusimama kwa muda mrefu wakati wa tendo.Tatizo hili husababishwa na vitu mbalimbali vikiwemo ajali,madawa,msongo wa mawazo 


 VIAGRA ZINAFANYAJE KAZI?...


 Viagra huongeza msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume na kuufanya usimame na uwe mgumu wa kujamiiana.Kwa kawaida viagra huanza kufanya kazi dakika 30-60 baada ya kumezwa na hutumika wakati mtu anataka kujamiiana.


  Baada ya tendo kumalizika uume unatakiwa utulie(loose erection) baada ya masaa manne endapo kama itazidi hapo muone daktari.


HUPASWI KUTUMIA VIAGRA KAMA:-


 i.Umetumia dawa zenye nitrates kama nitroglycerine


ii.Umetumia dawa zinazoitwa "poppers" kama amyl nitrate au amyl nitrite na butyl nitrate


iii.Una mzio (allergy) na viambatanisho (ingredients) zilizotumika kutengeneza viagra.


MADHARA YA VIAGRA:


i.Uume kusimama mda mrefu kupitiliza (priapism)


ii.Kupoteza uwezo wa kuona kwenye jicho moja au yote kwa ghafla


iii.Kupoteza uwezo wa kusikia ghafla


iv.Kupatwa na kizunguzungu


v.Maumivu ya kuchwa


vi.Maumivu ya misuli


vii.Mshtuko wa moyo (heart attack)


viii.Kiharusi (stroke)


ix.Kifo


Cc:@_afyazone






Post a Comment

0 Comments