Ticker

6/recent/ticker-posts

MAUMIVU YA TUMBO KWA MJAMZITO



 MJAMZITO

• • • • • •

MAUMIVU YA TUMBO KWA MJAMZITO


Zipo sababu mbali mbali ambazo huchangia kutokea kwa tatizo hili. Tatizo hili huwatokea wanawake wengi wajawazito kwa huvi sasa.


Kumbuka, baadhi ya sababu huweza kuwa hatarishi hata kwa ujauzito wenyewe, hivo huhitaji umakini zaidi na kutokuwa mtu wa kupuuzia mambo.


BAADHI YA SABABU AMBAZO HUWEZA KUCHANGIA MAUMIVU YA TUMBO KWA MAMA MJAMZITO NI PAMOJA NA;


1. Mimba kutunga Nje ya kizazi ambapo kwa kitaalam hujulikana kama ectopic pregnancy


2. Maumivu ya tumbo kwa sababu ya maambukizi ya magonjwa mbali mbali kama vile; PID,Fangasi,UTI,Kaswende,kisonono N.K


3. Mama mjamzito kuwa na shida ya uvimbe kwenye kizazi


4. Maumivu ya tumbo kutokana na mtoto alivyojishikiza kwenye ukuta wa mji wa mimba yaani Implantation process


5. Maumivu ya tumbo kutokana na shida ya kondo la nyuma kuachia ambapo kwa kitaalam hujulikana kama Placenta abruption


6. Maamivu ya tumbo kutokana na kondo la nyuma kushuka na kufunika njia ya mtoto kupita yaani Placenta praevia


7. Maumivu ya tumbo kutokana na mama mjamzito kulala vibaya. 


Mama mjamzito unashauriwa kulalia ubavu sio kifudifudi au vinginevyo, hasa hasa kulalia ubavu wako wa kushoto 


8. Maumivu makali ya tumbo kutokana na kupigwa ukiwa mjamzito hali ambayo huweza kuwa ni hatari kwako na kwa mtoto aliyetumboni

N.K



KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.








Post a Comment

0 Comments