Ticker

6/recent/ticker-posts

UGONJWA WA DAMU KUGANDA(chanzo,dalili,tiba)



 DAMU

• • • • •

UGONJWA WA DAMU KUGANDA(chanzo,dalili,tiba)


Katika hali ya kawaida ya mwili, huwa damu hutakiwa kuganda endapo kumetokea majeraha au hali yoyote ya kuchubuka mwili ambayo hufanya damu kutoka.


Endapo mwili haujapata jeraha lolote,ajali,au mchubuko wowote halafu damu ikaganda,hapo kuna tatizo, na huo ni ugonjwa kabsa wala sio hali ya kawaida.


Ugonjwa huu kwa kitaalam hujulikana kama thrombophilia na zipo sababu mbali mbali ambazo huchangia kutokea kwa ugonjwa huu.


CHANZO CHA UGONJWA HUU WA DAMU KUGANDA


• Kurithi vinasaba vya tatizo hili katika koo husika. Hivo basi kama kwenye familia yenu kuna tatizo hili,na wewe pia upo kwenye hatari ya kupatwa na tatizo hili la damu kuganda.


• Hitilafu katika protein za mwili wako ikiwa ni pamoja na upungufu wake kwa kiasi kikubwa, Mfano ni; Protein C,protein S,Prothrombin N.K


• Uwepo wa tatizo la kansa


• Hali ya vigandishi damu kufanya kazi kuliko kawaida yake au kwa kupita kiasi


• Kuwa na matatizo mengine ambayo hukufanya ukae sehemu moja kwa muda mrefu pasipo kufanya chochote mfano; watu wenye magonjwa ya kupooza N.K


• Kuwa na shida ya upungufu mkubwa wa vitamins aina ya vitamin B12 Na vitamin B6 mwilini.


• Kuwa na shida ya unene au uzito uliopitiliza.


DALILI ZA UGONJWA WA DAMU KUGANDA NI PAMOJA NA;


1. Mgonjwa kuhisi miguu kuwaka moto mara kwa mara


2. Mgonjwa kushindwa kupumua vizuri


3. Mgonjwa kupata tatizo la kukohoa makohozi ambayo yamechanganyika na damu


4. Joto la mwili la mgonjwa kuwa juu au mgonjwa kupata homa


5. Miguu ya Mgonjwa kubadilika rangi yake ya ngozi na kuwa myekundu


6.Mgonjwa kupata shida ya mapigo ya moyo kwenda mbio sanaa


7. Uwezo wa kuona kwa mgonjwa kupungua gafla


8. Mgonjwa kuhisi kichefuchefu na kutapika


9.Mgonjwa kupatwa na maumivu makali ya kichwa


10. Mgonjwa kutoa jasho sana kwenye mwili wake


MATIBABU YA UGONJWA WA DAMU KUGANDA


- Kuna vipimo vingi ambayo hufanyika kwanza kwa mgonjwa mwenye dalili hizi ikiwa ni pamoja na kipimo cha damu, kipimo cha kuangalia Utendaji kazi wa Protein mwilini,CBC, na vipimo vingine ndipo matibabu yaanze.


Hivo ni vizuri kwenda hospital mapema kama una tatizo hili au una dalili hizi ambazo nimezielezea kwenye makala hii.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.







Post a Comment

0 Comments