Ticker

6/recent/ticker-posts

DALILI ZA MTU MWENYE UPUNGUFU WA VITAMIN D Mwilini



 VITAMIN D

• • • • •

DALILI ZA MTU MWENYE UPUNGUFU WA VITAMIN D  Mwilini


Katika makala hii tunazungumzia tatizo la upungufu wa vitamin D mwilini yaani kwa kitaalam Vitamin D deficiency. Kwa  ujumla, vitamin mbali mbali ni muhimu sana kwenye mwili wako na kila aina ya vitamin ina kazi zake mwilini, hapa nazungumzia mfano; vitamin A, Vitamin B6, Vitamin C, Vitamin D, Vitamin B9, Vitamin B12 n.k


Upungufu wa vitamin D mwilini unasababishwa na nini? Na dalili zake ni zipi?(soma makala hii)


CHANZO CHA UPUNGUFU WA VITAMIN D MWILINI NI PAMOJA NA;


- Kula vyakula ambavyo havina vitamin D  kwa muda mwingi


- Kukaa mbali na jua kwa muda mrefu kwani utengenezaji wa vitamin D mwilini mwako hutegemea pia jua.


- Figo zako kushindwa kubadilisha vitamin D kuwa katika hali ya kutumika zaidi hasa kwa watu wenye umri mkubwa


- Kuwa na ngozi nyeusi sana, tafiti zinaonyesha melanini huweza kupunguza ngozi kutengeza vitamin D pale inapopigwa na jua


- Tatizo la mfumo wako wa umeng'enyaji kushindwa kufyoza vizuri vitamin D mbali na chakula unachokula chenye vitamin vya kutosha.


DALILI ZA UPUNGUFU WA VITAMIN D MWILINI


- Kupata maumivu ya mgongo mara kwa mara


- Kupata maumivu ya misuli,joint pamoja mifupa ya mwili mara kwa mara


- Kuwa na tatizo la vidonda kutokupona haraka


- Uchovu wa mwili kupita kiasi


-  kuwa na tatizo la Nywele kukatika sana na kunyonyoka zenyewe


- Watoto kuwa na shida ya matege


- Kushambuliwa na magonjwa mara kwa mara kutokana na kinga yako ya mwili kutokufanya kazi vizuri

N.k


TIBA YA UPUNGUFU WA VITAMIN D MWILINI


- Matibabu ya upungufu wa vitamin D mwilini huhusisha matumizi ya vyakula vyenye kiwango cha kutosha cha vitamin D, Dawa zakusaidia umeng'enyaji pamoja na ufyozwaji wa vitamin D mwilini, pamoja na matumizi ya Virutubisho mbali mbali yaani supplements


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments