Ticker

6/recent/ticker-posts

CHANZO CHA TATIZO LA MENO KUFA GANZI



 MENO

• • • • •

CHANZO CHA TATIZO LA MENO KUFA GANZI


Tatizo la meno kufa ganzi hutokana na kuathiriwa kwa mfumo wa nerves pamoja na kumomonyoka kwa kuta za enameli, hali hii hutokana na sababu mbali mbali kama vile;


1. Kula vitu vya baridi sana kama Barafu


2. Matumizi ya baadhi ya vinywaji kwa kiwango kikubwa Mfano; Mvinyo, hali ambayo hupelekea kuathirika kwa sehemu ngumu ya jino maarufu kama enameli


3. Kuwa na tabia ya kupenda kung'ata vitu vigumu hovio kama vile; Kalamu n.k, au wale ambao hupenda kufungua visoda vya vinywaji mbali mbali kama soda au bia kwa kutumia meno.


4. Kuwa na tabia ya kupenda kung'ata kucha kila mara


5. Wale ambao hupenda kula vitu kama Mirungi muda wote


6. Kusafisha meno kwa kutumia nguvu sana wakati wa kupiga mswaki


7. Kupatwa na tatizo la kusaga meno ambapo kwa kitaalam hujulikana kama Bruxism, tatizo ambalo huwapata sana watoto wadogo kuanzia mwaka 1 mpaka miaka 11.


8. Uvutaji wa Sigara


9. Matumizi ya Kahawa kwa kiwango kikubwa


10. Matumizi ya sukari kwa kiwango kikubwa au kupendelea kula vitu vyenye sukari sana

N.K


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments