Ticker

6/recent/ticker-posts

DAWA ZA MINYOO KWA MWANAMKE/MAMA MJAMZITO



 MJAMZITO

• • • • •

DAWA ZA MINYOO KWA MWANAMKE/MAMA MJAMZITO


Kama umewahi kwenda na kuhudhuria kliniki ukiwa mjamzito,utakubaliana na mimi kwamba wakina mama Wajawazito hupewa dawa zinazoitwa MEBENDAZOLE,


Je dawa hizi ni kwa ajili ya nini?


Wakina mama wajawazito hupewa Dawa za MEBENDAZOLE KWA AJILI YA TATIZO LA MINYOO


Je kwanini wanawake wajawazito Wasipewe ALBENDAZOLE ambazo watu wengi hutumia kwa ajili ya kutibu Minyoo?


UTAFITI: 


Baada ya utafiti kufanyika ambao ulihusisha panya pamoja na Sungura wajawazito,ulionyesha matumizi ya Albendazole huweza kuleta madhara kwa viumbe ambavyo vipo tumboni,


Japo hakuna ushahidi wa moja kwa moja kwa Binadamu.



Hivo basi, kutokana na utafiti huo ikaonekana chaguo bora zaidi kwa mama mjamzito iwe ni mebendazole badala ya Albendazole


KUJUA kuhusu MAHUDHURIO YA KLINIKI kwa Mama mjamzito,Soma hapa


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.







Post a Comment

0 Comments