Ticker

6/recent/ticker-posts

UGONJWA WA Q FEVER(chanzo,dalili,madhara na Tiba)



 Q FEVER

• • • • •

UGONJWA WA Q FEVER(chanzo,dalili,madhara na Tiba)


CHANZO


Ugonjwa wa Q fever ni ugonjwa ambao husababishwa na bacteria wanaojulikana kwa jina la Bacterium Coxiella Burnetii,


Bacteria hawa husambazwa kwenda kwa binadamu kupitia wanyama kama vile; Mbuzi,kondoo n.k


DALILI ZA UGONJWA WA Q FEVER NI PAMOJA NA;


✓ Joto la mwili kuwa juu sana Mfano; 41 °C


✓ Mgonjwa kupata tatizo la kuharisha


✓ Kupata kichefuchefu pamoja na kutapika


✓ Mgonjwa kukohoa mara kwa mara


✓ Mwili kutetemeka


✓ Mwili kuchoka kupita kawaida


✓ Mgonjwa kupata maumivu makali ya Kichwa



MADHARA YA UGONJWA WA Q FEVER


- Ugonjwa huu huweza kuharibu Mapafu,Ubongo,Ini pamoja na Moyo


- Ugonjwa huu huweza kusababisha kuvimba kwa kuta za ndani ya moyo yaani kwa kitaalam Endocarditis


- Ugonjwa huu huweza kusababisha shida kwenye mapafu kama vile; Pneumonia n.k


- Ugonjwa huu huweza kusababisha matatizo mbali mbali kwenye ujauzito kama vile;mimba kutoka zenyewe,mtoto kuzaliwa kabla ya wakati(premature), mtoto kuzaliwa na uzito mdogo,mtoto kuzaliwa mfu n.k


MATIBABU YA Q FEVER


• Ugonjwa huu huweza kutibiwa kwa kutumia dawa mbali mbali kama vile; Doxcycline n.k


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments